• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

RAIS Magufuli atoa msaada wa milioni tano kwa mwenye ulemavu Songea

Tarehe ya kuwekwa: July 5th, 2019

RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.John Magufuli ametoa msaada wa shilingi milioni tano kwa Mwenye ulemavu wa viungo Konsaluva Lungu mkazi wa Mshangano  Manispaa ya Songea.

Fedha hizo zimekabidhiwa kwa Konsaluva kwa niaba ya Rais na Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Christina Mndeme katika hafla iliyofanyika katika Benki ya CRDB tawi la Songea.

Mndeme amesema kitendo cha Rais kutoa msaada kwa mwenye ulemavu huyo kumedhihirisha kuwa ni Rais wa wanyonge na kwamba anawapenda watanzania na kuwajali.

Mndeme amesema Rais Magufuli baada ya kuona taarifa ya Konsaluva kwenye vyombo vya habari akifanyakazi kwa kujituma licha ya kuwa na ulemavu,aliguswa na kuamua kumsaidia.

“Mheshimiwa Rais anatambua kuna wenye ulemavu wapo wengi ndani ya nchi,lakini  alipendezwa namna Konsaluva alivyokuwa mbunifu kwa kufanyakazi na kulea mtoto wake bila wasiwasi’’,alisema.

Ametoa wito kwa wenye ulemavu kuacha kutumia ulemavu kama kigezo cha kuombaomba,badala yake watumie ulemavu kama changamoto hivyo wafanye kazi kwa bidii.

Mndeme amesema fedha hizo zitumike kununua cherehani kwa kuwa Konsaluva amejifunza ufundi kushona katika Chuo cha VETA Songea na kwamba fedha hizo zinaweza pia kumsaidia katika mambo mengine ya kujikimu na uzalishajimali.

Licha ya fedha hizo,Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma amesema serikali itampatia kiwanja na  kumpatia kibanda bure cha kufanyia biashara  ambako ataweka cherehani yake na kwamba amehamishwa toka na kupelekwa katika nyumba yenye mazingira rafiki yenye huduma za maji na umeme.

Konsaluva Lungu ni Mwenye ulemavu wa viungo tangu kuzaliwa akiwa na mguu mmoja,hana mikono na amewekewa mguu wa bandia, amemshukuru Rais kwa msaada huo na ameahidi kufanyakazi kwa bidii.

Konsaluva amevishukuru vyombo vya habari kwa kumuibua na kutangaza habari zake hali iliyosababisha Rais kumuona na kumsaidia na kwamba baada ya kupata msaada huo atajituma katika kufanyakazi.

“Namshukuru Mungu  na Rais Magufuli kwa kuniona,ameniambia kwamba nimpende Mungu na kila kitu ninachokifanya nimtangulize Mungu, Nakuahidi Rais Magufuli nitafanya kadiri ulivyonielekeza’’,alisisitiza Konsaluva.

Naye Meneja wa CRDB tawi la Songea Efrasiana  Mwanja akizungumza baada ya kufungua akaunti ya Konsaluva katika Benki hiyo,amempongeza Rais kwa moyo wa upendo kwa watanzania.

Sisi sote tulitamani baba zetu wote wawe na moyo kama wa mheshimiwa Rais Magufuli,sisi kama Benki ya CRDB  tumemuona Konsaluva ana mtoto mdogo tunamfungulia akaunti ya Junior Jumbo ,tutaanza na shilingi 100,000’’,alisisitiza.

Imeandikwa na Albano Midelo

Afisa Habari Manispaa ya Songea 

Juni 5,2019

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa