• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

RC IBUGE ATOA MAAGIZO KWA WADAU WA USAFIRISHAJI RUVUMA.

Tarehe ya kuwekwa: August 5th, 2021

Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Brigedia Jenerali Wilbert Ibuge amewataka wadau wa usafirishaji Mkoani Ruvuma kuzingatia muongozo uliotolewa na Wizara ya afya katika kukabiliana na wimbi la tatu la UVIKO 19.

Hayo yamebainishwa leo tarehe 05.08.2021 alipokutana  na wadau wa usafirishaji pamoja na viongozi mbalimbali Mkoani Ruvuma katika ukumbi wa Manispaa ya Songea kwa lengo la kujadiliana namna ya kupunguza maambukizi ya UVIKO 19 katika Nyanja ya usafirishaji.

Ibuge ameagiza vyombo vyote vya usafiri kuhakikisha wanabeba abiria kulingana na idadi inayotakiwa pamoja na kunatumia vifaa kinga ikiwemo na vipukusa mikono  ndoo za maji tiririka kwenye maeneo yote ya stendi  na kuhamasisha uvaaji wa barakoa kwa abiria wote wanaotumia vyombo hivyo vya usafiri kama vile mabasi, daladala, bajaji na bodaboda.

Ameongeza kuwa viongozi wa Halmashauri ya Manispaa ya Songea wanatakiwa kuweka misimamo ya msingi katika maeneo ya stendi ya Mfaranyaki, Ruhuwiko na Seedfarm ambazo zinatakiwa kutumika kwa ajili ya kushusha abiria  na kuitaka stendi ya Shule ya Tanga itumike ipasavyo kwa kupakia na kushusha abiria jambo ambalo litapunguza msongamano wa watu na vilevile kuiendeleza stendi kuu ya mabasi Shule ya Tanga.”Alisisitiza”

Amewataka wakala wa barabara Ruvuma (TANROADS) kuhakikisha wanakamilisha ujenzi wa wa daraja la Bombambili kwa muda hadi kufikia Septemba 10, 2021 ili kuondoa adha ya usafiri kwa abiria na watumiaji wa barabara hiyo.

Pia amemtaka Mganga Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma kwa kushilikiana na vyombo vya mawasiliano kuhakikisha anaweka mkakati wa kutoa elimu kwa umma kuhusiana na namna ya kujikinga na ugonjwa wa UVIKO 19 pamoja na umuhimu wa kupata chanjo ya ugonjwa huo kwa hiyari.”Alieleza” 

Ibuge amewasisitiza wadau wote wa usafirishaji Mkoani Ruvuma kuzingatia na kutii sheria za barabarani ikiwemo na kufunga mikanda na endapo kutakuwa na ukiukwaji wa sheria hizo hatua kali zichukuliwe na mamlaka husika.

IMEANDALIWA NA,

AMINA PILLY,

AFISA HABARI MANISPAA,

05.08.2021.

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa