• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

RC Ruvuma Afanya Ziara ya Kushitukiza katika Soko la Bombambili, Atoa Maagizo ya Muda wa Siku 14 Kwa Halmashauri.

Tarehe ya kuwekwa: August 1st, 2025

Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma, Kanal. Ahmed Abbas Ahmed leo amefanya ziara ya kushtukiza katika soko la Bombambili lililopo Manispaa ya Songea kwa lengo la kusikiliza na kutatua kero zinazowakabili wafanyabiashara wa soko hilo.

Katika ziara hiyo iliyofanyika tarhe 01 Agosti 2025, Kanal Ahmed aliwataka wananchi kutumia fursa wanapokutana na viongozi kutoa kero zao moja kwa moja ili zipatiwe majibu na ufafanuzi wa papo kwa papo, badala ya kunung’unika bila hatua kuchukuliwa.

“Niwapongeze kwa kazi mnayoifanya. Serikali ipo bega kwa bega nanyi, tunahitaji kujua changamoto zenu ili tuweze kuzitatua kwa wakati,” alisema Kanal Ahmed.

Baada ya kukagua mazingira ya soko na kusikiliza kero za wafanyabiashara, alibainisha changamoto mbalimbali ikiwemo uchafu wa mazingira, miundombinu ya barabara kuwa mibovu, na mlundikano wa wafanyabiashara bila mpangilio rasmi.

Kutokana na hali hiyo, Mkuu huyo wa Mkoa alitoa maagizo kwa wataalamu wa Halmashauri ya Manispaa ya Songea kuhakikisha ndani ya siku 7 wanawapanga wafanyabiashara kwa utaratibu mzuri, na pia kuweka mikakati madhubuti ya usafi wa mazingira.

Aidha, alitoa agizo la kutekeleza zoezi la kuchonga barabara zinazozunguka soko hilo ndani ya siku 14, akisisitiza kuwa utekelezaji huo ni wa lazima kwa maendeleo ya eneo hilo la biashara.

“Usafi hauridhishi. Mlundikano wa wafanyabiashara unaonesha kutopangwa, kuna maeneo yameachwa wazi pasipo matumizi. Miundombinu ya barabara ni mibovu na kuna uchafu wa mazingira,” alifafanua Kanal Ahmed.

Kuhusu mikopo ya asilimia 10 kutoka Halmashauri, aliagiza wataalamu waendelee kutoa elimu kwa makundi mbalimbali ya jamii ikiwemo madereva wa bodaboda, bajaji, mama lishe na wajasiriamali wadogo ili waweze kunufaika.

Katika hatua nyingine, alitoa maagizo kwa Halmashauri kuhakikisha maduka yote yaliyofungwa kwa sababu ya kutolipa ushuru yafunguliwe, huku wakiweka utaratibu wa wafanyabiashara kulipa kwa awamu.

“Wale wote mliowafungia kwa sababu ya kudaiwa, wafungulieni maduka yao. Wekeni utaratibu wa kulipa kwa awamu hadi wakamilishe,” alisisitiza Mkuu wa Mkoa.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Songea, Mhe. Kapenjama Ndile alitoa wito kwa wananchi kudai utekelezaji wa miundombinu, akibainisha kuwa baadhi ya changamoto zinahitaji hatua zaidi ikiwemo uvunjaji wa nyumba na uondoshaji wa makaburi yaliyopo kwenye maeneo ya miundombinu, zoezi ambalo linakadiriwa kugharimu takriban Shilingi milioni 197.

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA July 08, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 July 04, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • RC Ruvuma Afanya Ziara ya Kushitukiza katika Soko la Bombambili, Atoa Maagizo ya Muda wa Siku 14 Kwa Halmashauri.

    August 01, 2025
  • Dkt. Samia Awasili Ruvuma.

    July 30, 2025
  • Mhe. Jenista Waziri wa Afya; Serikali yapambana kupunguza Maambukizi Mapya ya Virus vya Homa ya INI.

    July 29, 2025
  • Songea MC Yadhamiria Kuboresha Lishe na Kuondoa Udumavu

    July 25, 2025
  • Tazama zote

Video

RC Ruvuma Asikiliza na kutatua Kero za Wafanyabiashara
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa