• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

RC RUVUMA AIPONGEZA MANISPAA YA SONGEA KUPATA HATI SAFI.

Tarehe ya kuwekwa: June 24th, 2022

Na,

AMINA PILLY,

AFISA HABARI MANISPAA.

26 JUNI 2022

Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Brigedia Jenerali (Balozi) Wilbert Ibuge ameitaka Halmashauri ya Manispaa ya Songea kubuni vyanzo vipya vya mapato ili waweze kuwa na wigo mkubwa katika ukusanyaji wa mapato ya ndani.

Ameyasema hayo leo wakati wa kikao cha Baraza maalum la Madiwani kupitia na kujadili taarifa ya mdhibiti mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) kwa mwaka wa fedha 2020/2021.

“Pamoja kupata hati safi ninatoa rai kwa Mkurugenzi mtendaji na timu ya wataalamu kuhakikisha mnaimarisha usimamizi wa ukusanyaji wa mapato ya ndani pamoja na kuboresha matumizi ya fedha hizo lakini pia kuendelea kubuni vyanzo vipya vya mapato” Alibainisha.

Brig. Ibuge amewataka viongozi wa Halmashauri ya Manispaa ya Songea kuhakikisha wanafunga hoja zote kufikia Juni 30 mwaka huu pamoja na kuzuiauwepo wa  hoja za nyuma ambazo hujirudia mara kwa mara ambapo amesema wakuu wa Idara wote wanatakiwa kushiriki ipasavyo katika kuandaa majibu ya hoja na kufanyia kazi maelekezo ya CAG.

Aidha, amewataka Madiwani wote, kuhakikisha wanadhibiti mianya ya upotevu wa mapato ya Serikali pamoja na kufuatilia suala la utoaji mikopo ya 10%  kwa wanawake 4%, vijana 4%, na watu wenye ulemavu 2% na kufuata sheria na kanuni ili mikopo hiyo irejeshwe kwa wakati na kuwezesha wengine kunufaika na mikopo hiyo“Alisisitiza”


Ametoa rai kwa Madiwani kuhakikisha wanatimiza wajibu wao kwa wananchi kwa kusimamia utekelezaji wa miradi ya maendeleo pamoja na kuchukua hatua za kinidhamu mapema kwa watumishi wasiotimiza wajibu wao kwa kufuata kanuni na misingi ya utawala bora.

Mkuu wa Wilaya ya Songea Pololet Kamando Mgema alianza kwa  kuipongeza Halmashauri ya Manispaa ya Songea kwa kuweza kupata hati safi, hivyo amewataka wataalamu hao  kuelekea mwisho wa mwaka wa fedha kila Halmashauri  ihakikishe inapokea taarifa kutoka kwa mdhibiti mkuu wa hesabu za Serikali na kuzifanyia kazi kwa usahihi.


Kwa upande wake Mkaguzi Mkazi wa Mkoa wa Ruvuma Deogratius Waijaha amewataka viongozi kuhakikisha wanamalizia ujenzi wa bwalo la chakula katika shule ya Sekondari ya Emmanuel Nchimbi ili lianze kutumika pamoja na kufuatilia hati miliki ya viwanja vya masoko 7 na stendi 2 za mabasi.


Naye mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Hamisi Abdallah Ally amewataka Madiwani kuendelea kuunga mkono maono ya Serikali ya Awamu ya sita kwa kutimiza wajibu wao wa kuleta maendeleo kwa wananchi waliowachagua pamoja na kuhakikisha wanasimamia shughuli zote za maendeleo pamoja na usimamizi wa ukusanyaji wa mapato ya ndani kuhakikisha unavuka malengo ya Halmashauri waliyojiwekea.

Akihitimisha Baraza hilo Mstahiki Meya Manispaa ya Songea Michael Mbano alibainisha kuwa kwa mujibu wa taarifa ya fedha iliyotolewa tarehe 31 Marchi 2022 makusanyo ya mapato ndani kwa Halmashauri tayari yamevuka lengo walilojiwekea kwa zaidi ya asilimia 100% pamoja na utoaji wa fedha asilimia 10% za mapato ya ndani kwa vikundi ambapo sh. Million 700 tayari zimeshatolewa.  

Mwisho. 

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa