• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

RC RUVUMA AKEMEA UOVU TASAF AMESEMA 'UKIZINGUA TUTAZINGUANA'.

Tarehe ya kuwekwa: April 20th, 2021

TASAF ni chombo cha serikali kilichoundwa kwa lengo la kusaidia jitihada za wananchi katika kuondoa kero ya umaskini, kukuza uchumi na kuongeza kipato, kuboresha huduma za jamii na kuendeleza watoto wanaoishi kwenye kaya za  walengwa katika sekta ya elimu, afya na lishe.

Ili kufanikisha Mipango hiyo, TASAF imefanya kikao kazi kwa wataalamu  kwa lengo la  kuwajengea uelewa juu ya utekelezaji wa kipindi cha pili cha awamu ya tatu ya TASAF kinachofanyika   katika ukumbi wa Manispaa ya Songea kuanzia 19-23 Aprili 2021 na kuhudhuriwa na Waheshimiwa Madiwani na  Wataalamu  na viongozi mbalimbali Manispaa ya Songea.

Mgeni rasmi katika mafunzo hayo alikuwa Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Christina Mndeme ambaye katika hotuba yake ya ufunguzi wa kikao hicho alisema “ tathimini ya utekelezaji wa kipindi cha kwanza cha awamu ya tatu ya TASAF  kinaonesha kuwa Mpango huu  umechangia kwa kiasi kikubwa  kufikia lengo la Serikali la kupunguza umaskini nchini kukiwa na takwimu zinazoonesha utekelezaji wa Mpango kwenye kipindi cha kwanza awamu ya tatu  Mkoani Ruvuma wenye wanufaika 44,836.”

Mndeme ametoa wito  kwa washiriki wote wa mafunzo hayo kufanya kazi kwa weredi ili kufanikisha kutekeleza Mpango wakuibua kaya lengwa ambapo alisema  endapo  atagundua  kama kuna ongezeko la kaya hewa  ambazo zitawekwa kwa upendeleo wowote hatua kali za kisheria  zitachukuliwa dhidi yao “alisema ukizingua tutazinguana”.  ‘Alisisitiza’

Akitoa pongezi kwa Mkurugenzi wa Manispaa ya Songea Tina Sekambo pamoja na timu ya wataalamu wa Manispaa ya Songea  kwa kupata hati inayoridhisha. Hata hivyo ametoa  rai kwa wafanyabiashara wote Mkoani Ruvuma  kuhakikisha wanauza bidhaa zao  kwa  bei  nafuu hasa katika msimu huu wa Ramadhani na endapo itabainika  kuna mfanyabiashara yeyote amepandisha bei kwa maslahi binafsi hatua kali za kisheria zitachukuliwa dhidi yao.

Naye  Kaimu Meneja wa mpango wa kukuza uchumi TASAF Catherine Kissanga alisema  mafanikio  yaliyofikiwa katika kipindi cha kwanza ni asimilia 70% ya vijiji/mitaa/shehia zote nchini hivyo bado kuna wananchi wanaoishi katika hali duni kwenye maeneno ambayo hayakufikiwa.

Kisanga alisema Kipindi cha pili kilianza kwa uhakiki wa walengwa wote na kuondoa kaya zote za walengwa ambazo zimepoteza sifa mara baada ya kujitokeza kwa malalamiko mengi kuhusu Mpango kuwa na watu wasiostahili wakiwemo watu wasio maskini, viongozi, orodha ya watu waliohama au waliofariki ambao wote ni walengwa hewa.

Alisema kipindi cha pili cha awamu ya tatu TASAF ambacho kitatekelezwa katika halmashauri zote 184 za Tanzania Bara na Wilaya zote za Zanzibar, na kufikia  kaya milioni moja laki nne na nusu  zenye jumla ya watu milioni 7 nchini  ikiwa ni nyongeza ya kaya laki tatu na nusu kutoka kwenye kipindi cha kwanza cha Mpango huo.

Kisanga alibainisha  kuwa jumla ya kaya lengwa 4221 Manispaa ya Songea zimefikiwa na TASSAF  ambapo  Mpango huu utaendelea kusaidia  kaya zenye  hali duni kwenye vijiji, mitaa na shehia zote ambazo Mpango huu unawezesha kaya maskini hasa watoto wenye umri chini ya miaka mitano 5 ambao wanahudhiria kliniki,  wanafunzi wanaosoma shule za awali,  shule za msingi na shule za sekondari, akina mama wajawazito pamoja na kaya zenye ulemavu na  uhakikisha wanapata lishe bora,  huduma za afya na elimu.

Alibainsha kuwa ili kuwajengea uwezo Wawezeshaji watakaosimamia Mpango wa kipindi cha pili cha Awamu ya tatu TASAF watapatiwa mafunzo na  kusaini viapo vya uadilifu na  kisha watatakiwa kushiriki kwenye zoezi la uibuaji wa  kaya lengwa katika vijiji/Mtaa/Shehia.

 ‘Kisanga alisisitiza’.

Naye Mstahiki Meya wa Manispaa ya Songea Michael Mbano amewataka Waheshimiwa Madiwani Manispaa ya Songea kuleta ushirikiano kwa wataalamu watakao shiriki katika kuibua kaya lengwa na  kuhakikisha  usimamizi wa Mpango wa TASAF wa kipindi cha pili unawafikia walengwa waliokusudiwa.

Nao washiriki wa mafunzo hayo wakitoa pongezi kwa Serikali  kwa kuwawezesha mafunzo ambayo yatawasaidia kuwajengea uwezo wa kufahamu kuhusu namna ya kuibua kaya maskini  katika kipindi cha pili Awamu ya tatu TASAF ambacho kinalenga kuongeza mitaa 36 mipya ambayo haikufikiwa kwenye kipindi cha kwanza Manispaa ya Songea.

 

IMEANDALIWA NA;

AMINA PILLY;

AFISA HABARI MANISPAA YA SONGEA.

20 APRILI 2021   

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa