• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

RC RUVUMA ATOA AGIZO KWA WAWEKEZAJI WA MGODI WA MADINI YA MAKAA YA MAWE, " KULIPA DENI LA KODI WANAYODAIWA MIL. 274"

Tarehe ya kuwekwa: September 4th, 2020

Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Christina Mndeme ametoa agizo hilo  leo katika kikao chake cha utatuzi wa Mgogoro baina ya mwekezaji wa ndani na  mwekezaji wa nje wa Mgodi wa   Makaa ya Mawe unaomilikiwa na Kampuni ya ( MIL-COAL Songea), kilichofanyika katika ya Ofisi ya Mkuu wa Mkoa tarehe 04/09/2020.

Mndeme alisema” awali alipokea mgogoro wa Wawekezaji wa Mgodi wa makaa ya mawe unaotambulika kwa jina la Market Insigut Limited (MIC-COAL Songea) ambapo aliunda tume ya  Uchunguzi na hatimaye alibaini mapungufu ya kimkataba baina ya Mwekezaji wa ndani na mwekezaji wanje.

Alibainisha kuwa sambamba na changamoto iliyojitokeza tume hiyo imebaini uwepo wa  baadhi ya mapungufu yanayoikabili kampuni hiyo ya Madini pamoja na  Kampuni kutolipa kodi ya Serikali  zaidi ya Tsh milioni 274, Kutolipa mishahara ya Watumishi kwa wakati, pamoja na upotevu wa fedha za malipo yamishahara ya  wafanyakazi  zaidi  ya milioni 62 zilizochukuliwa na Fredrick Mwaipopo ambaye alikuwa mhandisi wa Kampuni hiyo.

Hata hivyo baada ya kutatua mgogoro huo, amewaagiza  Wawekezaji  hao kuanza kazi  rasmi leo ya  uchimbaji wa Makaa ya mawe, kulipa kodi wanayodaiwa Zaidi ya Milioni 274, kulipa madai yote ya Watumishi wanayodaiwa, kufungua ajira kwa Watanzania, kuuza makaa ya mawe kwenye viwanda vya ndani ili vipate nishati ya kutosha,  na kulipa kodi ya huduma              ( service leavy) ya Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga.  

Aidha, aliagiza kukamatwa kwa Fredrick Mwaipopo ( Mhandisi wa Kampuni)  ambaye anatuhumiwa kuhujumu uendeshaji wa Mgodi kwa kuchukua fedha milioni 62 ambazo zilikuwa malipo yamishahara ya  wafanyakazi wa Mgodi huo.

Naye Kaimu  Afisa madini Mkoa wa Ruvuma Jumanne M. Nkana alisema” baada ya kupokea malalamiko ya wawekezaji hao aliwaita na kusuluhisha kwa kufanya mapitio ya mkataba wao wa awali ambao mwekezaji wa ndani alikuwa anapata 30% na mwekezaji wa nje alikuwa anapata 70%, hata hivyo mkataba huo ulirekebishwa kwa awamu nyingine na  kukubaliana kuwa  mwekezaji wa ndani atapata 37.5% na mwekezaji wa nje atapata  62.5% ambapo bado mgogoro uliendelea na hatimaye walishauriwa kutumia utaratibu wa mwingine ambao unatumika kila tani inayouzwa lazima ilipwe kiasi cha fedha.”

Jumanne aliongeza kuwa,  Kampuni hiyo ilisimama kufanya kazi kwa muda mrefu kuanzia disemba 2019 na hii nikutokana na kuharibika kwa miundombinu ya barabara kuanzia eneo la mgodi hadi sehemu ya kuweka makaa ya mawe, na  baada ya kubaini hilo ililazimu kutengeneza miundombinu na hatimaye mwezi aprili 2020 Kampuni hiyo ilianza kusafirisha makaa ya mawe kutoka mgodini.  

Naye Mkuu wa Wilaya ya Mbinga Cosmas M. Nshenye alitoa ushauri kwa kampuni hiyo kuboresha vitendea kazi vya watumishi kama vile (Barakoa), kuboresha miundombinu, na malipo ya mishahara ya wafanyakazi.

IMETAYARISHWA NA;

AMINA PILLY;

AFISA HABARI MANISPAA YA SONGEA.

04.09.2020

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa