• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

RC RUVUMA ATOA MAAGIZO KWA WAKUU WA WILAYA.

Tarehe ya kuwekwa: June 22nd, 2021

“Uteuzi wa viongozi hawa unawataka kuja kusimamia  malengo ya serikali kwa kuhakikisha wananchi wanaishi sehemu salama.”

Kauli hiyo imetolewa leo tarehe 22 juni na  Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Brigedia Generali  Wilbert Ibuge  akiwa  katika usimamizi wa  zoezi la  utoaji kiapo  kwa Wakuu wa Wilaya ya Namtumbo Julius Keneth Ningu na Mkuu wa Wilaya ya Nyasa Col. L.E. Thomas kilichofanyika katika ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma na hudhuriwa na Makatibu Tawala Mkoa/ Wilaya, Wakurugenzi wa Halmashauri 8, Wazee wa Kimila, Viongozi wa dini pamoja na kamati ya ulinzi na usalama.

Ibuge alisema Lengo la serikali ni kuhakikisha uwepo wa ulinzi na usalama katika maeneo yao kwa  kuhakikisha   wananchi  wanakuwa salama pamoja na kuwashirikisha  wenyewe katika suala la  ulinzi  shirikishi  jamii kwa ajili ya maslahi yao binafsi na Nchi kwa ujumla.

Sambamba na uwajibikaji,  amewataka viongozi hao kusimamia maendeleo ya kiuchumi na kijamii ikiwemo na usimamizi wa miradi inayotekelezwa kwenye maeneo yao na kuhakikisha inakuwa yenye tija, yenye thamani ya fedha ambayo imetengewa  na kukamilishwa kwa kiwango kinachostahili. “ Ibuge alisisitiza”  

Alibainisha kuwa, fedha zitokanazo na mapato ya ndani wahakikishe inatengwa asilimia 10 kwa ajili ya kuwezesha makundi maalumu “wanawake 4%, vijana 4% na walemavu 2%” pamoja kusimamia vizuri urejeshwaji wa fedha hizo ambazo hazina riba ili ziweze kuwasaidia wanavikundi wengine.

Aliongeza kuwa kila kiongozi katika maeneo yake ahakikishe anahamasisha wananchi juu ya kujiunga na huduma ya  Bima ya Afya iliyoboreshwa CHF pamoja na kusimamia fedha zote zinazotakiwa kununuliwa  dawa zinawekwa Benk na dawa ziombwe kupitia mifumo inayoeleweka.  

Ibuge alisema Mkoa wa Ruvuma ni Mkoa adhimu ambao wananchi wake wanajituma nani Mkoa ambao hauna historia ya njaa kwani wananchi wenyewe hujizalishia chakula wenyewe na kujilisha. Hivyo amewataka wahakikishe wanasimamia mazao ya kimkakati na ya kibiashara  ambayo ni muhimu   kwa ajili ya kuongeza uzalishaji na kipato cha mtu mmoja mmoja.

Hata hivyo ametoa Rai kwa viongozi hao kuendelea kusimamia utekelezaji wa Sera kama zilivyoainishwa ikiwemo na utatuzi wa kero za wananchi, ambapo  alisema endapo kero za wananchi zitaachwa na kukomaa zitafifisha maendeleo ya wananchi.

Amewataka wananchi kuendelea kuchukua tahadhari juu ya ugonjwa wa homa kali ya mapafu ambao husababisha kushindwa kupumua, ambapo alisema ni bora kufuata maelekezo yanayotolewa na wataalamu wa afya kwani kinga ni bora kuliko tiba.

Naye Mkuu wa Wilaya ya Namtumbo Julius  Nungu alisema atafanyakazi kwa kushirikiana na wananchi na atategemea sana kujifunza kupitia kwao wananchi, ambapo alibainisha kuwa bila ya uwepo wa wao wananchi yeye si kiongozi.

Naye Mkuu wa Wilaya ya Nyasa  Col. L. E. Thomas  alisema hahitaji kuwa kiongozi mtawala bali atakuwa mtumishi wa wananchi wa Nyasa na atachukua changamoto zilizopo na kuzibadili kuwa fursa.

Naye Mganga Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma  Dkt. Jairy  Khanga alisema hatunabudi kuendelea kutoa elimu kwa wananchi juu ya wimbi la tatu la homa kali ya mapafu pia akiwataka wananchi kwa ujumla  kuchukua tahadhari na kuepuka Mikusanyiko isiyoyalazima au kuvaa barakoa, kunawa mikono kwa maji tiririka na kutumia vitakasa mikono.

Dkt. Khanga amegawa vipaza sauti kwa wakuu wa Wilaya kwa ajili ya kutoa elimu kwa wananchi juu ya homa kali ya mapafu. Amewaondoa hofu wananchi Mkoani Ruvuma kuwa hadi hivi sasa Mkoa upo salama hakuna mgonjwa yeyote au mhisiwa bali tuchukue tahadhari.

 

IMEANDALIWA NA;

AMINA PILLY;

AFISA HABARI MANISPAA YA SONGEA.

22 JUNI 2021.

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • MWENGE WA UHURU WAPOKELEWA MKOANI RUVUMA

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma Awapongeza Wastaafu 86 wa Kada ya Ualimu Mkoani Ruvuma

    May 08, 2025
  • Kamati ya Siasa Wilaya Yaridhishwa na Hatua za Miradi ya Maendeleo

    May 06, 2025
  • Tazama zote

Video

YALIYOJIRI MAKABIDHIANO YA MBIO ZA MWENGE WA UHURU
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa