• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

RC RUVUMA ATOA MAAGIZO MAZITO "Baraza la kwanza la Madiwani Manispaa ya Songea".

Tarehe ya kuwekwa: December 17th, 2020

Serikali za mitaa ni chombo kilichoanzishwa kisheria kwa mujibu wa Ibara ya 145 na 146 ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977 ambayo imetaja majukumu ya Serikali za mitaa katika Halmashauri yakiwa  yameainishwa katika sura ya 287.

Hayo yamebainika katika mkutano mkuu wa kwanza wa Uchaguzi wa Meya na Naibu Meya na wajumbe wa kamati za kudumu za Halmashauri ambapo kwa mujibu wa kanuni za uendeshaji wa mkutano wa kwanza wa Halmashauri  huongozwa na katibu tawala wa Wilaya.

Mkutano huo ulifunguliwa na Katibu Tawala Wilaya ya Songea  Pendo Daniel uliofanyika katika ukumbi wa Halmashauri ya Manispaa ya Songea kwa lengo la kuwapatia Madiwani hao tamko la maandishi,  kumchagua Meya na Naibu Meya, kuunda kamati za kudumu za Halmashauri, kupokea taarifa mbalimbali za utekelezaji wa shughuli za Halmashauri zilizofanyika katika kipindi ambacho baraza la madiwani lilivunjwa pamoja na kiapo cha uadilifu.

Awali Madiwani hao walitoa Tamko la maandishi na kiapo cha uadilifu kilichotolewa mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu Mfawidhi wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Songea Livini B. Lyakinana.

Pendo Katika  hotuba yake ya ufunguzi iliyosomwa  mkutanoni hapo  nanukuu” shughuli na maamuzi katika serikali za mitaa hufanywa  kupitia mikutano na vikao ambavyo huongozwa kwa kanuni za kudumu zilizoizinishwa na Waziri mwenye dhamana za Serikali za mitaa ikiwa imekataza  kutokuwepo kwa migogoro na migongano miongoni mwa madiwani wenyewe na watendaji wa mamlaka.” Mwisho wa kunukuu. 

Akitangaza matokeo ya  uchaguzi baada ya zoezi la upigaji kura wa kumchagua Meya na Naibu Meya ambapo Michael Leodgar Mbano  alipata kura 28, kura zilizoharibika (hakuna),  kura zilizokataliwa (hakuna), kura za ndiyo ni 28, hatimaye ndugu Michael L. Mbano alitangazwa kuwa Meya wa Manispaa ya Songea. Hatua ya pili ilikuwa ya kumchagua Naibu Meya ambapo kura zilizoharibika  (hakuna), kura zilizokataliwa (hakuna), kura za ndiyo ni 28 na hatimaye ndugu Jeremia Green Mlembe kutangazwa kuwa Naibu Meya Manispaa ya Songea.” Pendo alitamka.”

Baada ya kutangazwa kwa matokeo ya ushindi  wa nafasi ya Meya na Naibu Meya kwa pamoja viongozi hao walitoa shukrani kwa chama cha mapinduzi kwa kuwateua kugombea nafasi hizo walizozipata wakisisitiza kufanya kazi kwa  kushirikiana baina ya Madiwani wenzao, wananchi waliowachagua pamoja na wataalamu kufanya kazi kwa weledi kwa kuzingatia kanuni, miongozo, na taratibu zilizowekwa na Serikali.

Naye Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Christina Mndeme  akihutubia baraza hilo kwa mara ya kwanza alilipongeza baraza lililomaliza muda wake 2019-2020 kuwa walifanya kazi nzuri ya kukusanya mapato na kufikia 99%, amewaasa Madiwani hao kuongeza jitihada za ukusanyaji wa mapato kuanzia 99%  hadi 100% ifikapo june 2020-2021.

Mndeme amewataka madiwani hao  kusimamia kituo kipya cha mabasi cha Tanga kuanza  kufanya  kazi ifikapo 31 disemba 2020,  Machinjio mpya ya Tanga  ianze kufanya kazi kabla ya tarehe 1 Januari 2021,  kuhamasisha wafanyabiashara kulipa kodi kwa maendeleo ya Taifa letu, kufungua kiwanda kipya cha utengenezaji wa bidhaa za ngozi, pamoja na ujenzi wa  hospitali ya Rufaa  Mkoa wa  Ruvuma.

Alisema haoni sababu ya msingi ya kutofanya kazi kituo kipya cha mabasi cha Tanga kukiwa kuna eneo la kupaki daladala, eneo la kupaki bodaboda na bajaji , eneo la kupaki tax, “ pamoja na uwepo wa  vibanda 30 vya wafanyabiashara, vibanda 20 vya kukatia tiketi, na huduma ya bafu na vyoo ambayo hupatikana kituoni hapo. “ Alisisitiza”

 Mwisho, amewaasa wajumbe wa kamati ya fedha kusimamia miradi ipasavyo ikiwemo na ufungaji wa mashine ya machinjio ya nyama ili iweze kuongeza ajira kwa kwa jamii.

IMETAYARISHWA NA;

AMINA PILLY;

AFISA HABARI MANISPAA YA SONGEA.

16 Disemba 2020.

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa