• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

RC RUVUMA KUIPONGEZA MANISPAA YA SONGEA KWA ONGEZEKO LA MAPATO YATOKANAYO NA STENDI YA TANGA.

Tarehe ya kuwekwa: January 13th, 2021

NAIPONGEZA Halmashauri ya Manispaa ya Songea kwa kufaulisha kwa asilimia 85.51.  Aidha, halmashauri ya Wilaya ya Songea inatakiwa kuongeza juhudi ili  kupandisha  ufaulu zaidi kwani matokeo yanaonesha wamefaulisha kwa asilimia 66.68.

 

Hayo yamebainishwa na Mkuu wa Mkoa Wa Ruvuma Christina Mndeme akiwa katika kikao cha kamati ya Ushauri Mkoa wa Ruvuma kilichofanyika tarehe 12 januari 2021 katika ukumbi wa Manispaa ya Songea.

Mndeme alianza  kutoa  shukrani  kwa Wananchi wa Mkoa wa Ruvuma kwa kuunga mkono juhudi za Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Joseph Magufuli za kuwaletea maendeleo Watanzania wote, na Hii imejidhihirisha wakati wa  maandalizi ya Uchaguzi na Uchaguzi Mkuu wa 2020  kwa kuhakikisha Chama cha Mapinduzi Mkoa wa Ruvuma kinashinda kwa asilimia 84.1 kwa nafasi ya Rais, asilimia 78.2 kwa nafasi ya Ubunge na kufanya Majimbo yote tisa (9) kuwa miongoni mwa CCM na Kata 170 sawa na asilia 98.3.  Ama hakika Ushindi huu ni mkubwa mno na haijawahi kutokea toka mfumo wa vyama vingi uanze “Hongereni sana!!.”

Akizungumzia kuhusu Elimu alisema  matokeo ya kidato cha sita mwaka 2020, Mkoa umefanya vizuri kwa ufaulu wa asilimia 98.8.  Miundombinu kwa ajili ya wanafunzi wa kidato cha kwanza 2021, Takwimu zinaonesha hadi kufikia Novemba, 2020 kulikuwa na upungufu wa vyumba vya madarasa 43 kwa ajili ya kidato cha kwanza 2021.  Ameagiza Halmashauri zote kuhakikisha wanafunzi wote waliofaulu wanaanza masomo Januari, 2021 na  hakuna mtoto atakaebaki nyumbani kwa kukosa nafasi.  

 

Aliongeza kuwa Mkoa wetu unatekeleza kampeni ya Magauni manne chini ya Kaulimbiu ya “Niache Nisome” ambapo Serikali ya Mkoa wa Ruvuma kwa kushirikiana na wadau mbalimbali wa elimu inapambana na kuhakikisha inaondoa na kumaliza vikwazo vinavyosababisha wanafunzi wa kike kushindwa kuhudhuria na kudumu shuleni ikiwemo kushindwa kumaliza masomo kutokana na mimba za utotoni. “ Alisisistiza”.

Alisema Katika msimu huu wa kilimo wa mwaka 2020/2021 umelenga kulima hekta 672,137 za mazao ya chakula, Biashara na mazao ya bustani na kutarajia kuvuna tani 1,790,582, ambapo Mafanikio ya uzalishaji katika kilimo yanatokana na matumizi bora ya pembejeo za kilimo. Alibainisha kuwa, Serikali katika msimu huu 2020/2021 itaendelea na mfumo wa bei elekezi kununua pembejeo za kilimo hususan mbolea ya kupandia (DAP) na ya kukuzia (UREA).  Pia Wizara ya kilimo pamoja na mamlaka ya udhibitii wa ubora wa mbolea Tanzania (TFRA) imetoa bei elekezi kwa kila Wilaya hapa Mkoani Ruvuma. 

Aidha, Mkoa unaendelea kushirikiana na taasisi zingine za Serikali katika kusimamia zoezi la ununuzi wa Korosho kutoka kwa wakulima.  Hadi sasa jumla ya kilo 14,826,644 za  ya Korosho zenye thamani ya Tshs 33,893,774,357.00 zimeuzwa na minada inaendelea.

 

Akiipongeza Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru  kwa kukusanya Mapato ya Ndani kwa 121.87% pamoja na  Halmashauri ya Manispaa ya Songea tangu imeanza kutumia stendi kuu ya Shule ya Tanga  tarehe 01 Januari, 2021 imeongeza ukusanyaji wa mapato ya ndani  yatokanayo na ushuru wa stendi na choo kutoka Tshs. 400,000 hadi Tshs. 900,000 kwa kila siku, kwa mwezi tunategemea Manispaa itakusanya zaidi ya Tshs. 27,000,000/=.

Alisema TRA kwa kazi nzuri wanayoifanya ya kukusanya Mapato ndani ya Mkoa mwaka 2019/2020, tumeweza kukusanya Tshs. 15,885,857,987.22 sawa na 94% na kwa kipindi cha nusu ya kwanza ya mwaka wa fedha 2021, TRA imekusanya jumla ya Tshs. 16,365,091,735.82 ambayo ni sawa na 105%. Hongereni sana.

 

Naye Mganga Mkuu Mkoa wa Ruvuma Jairy Khanga akitoa ufafanuzi juu ya CHF iliyoboreshwa ambapo alisema CHF iliyoboreshwa  ilianzishwa mwezi septemba mwaka 2019  hadi kufikia disemba 2019 Mkoa wa Ruvuma ulikuwa umesajili kaya 2500, na hadi kufikia 2020 disemba Mkoa wa Ruvuma umesajili  kaya 11,295 kukiwa na asilimia 10.5, kwa hiyo ili suala hili liweze kutekelezwa kwa ufasaha inabidi itolewe elimu ya kutosha kwa wananchi  kuhusu CHF iliyoboreshwa.

Khanga alisema ni Wilaya ya Tunduru katika kituo cha Matemanga pekee wamejitahidi kudai tofauti na vituo vingine hushindwa kudai madai kwa wakati.na kupelekea kukosekana kwa baadhi ya huduma za afya.

Amezitaka Halmashauri zote Mkoani Ruvuma kuwaagiza waganga wakuu wa kila Halmashauri kuhakikisha wanawaandika barua kwa wasimamizi wa kila kituo cha Zahanati/Kituo cha Afya  kwaajili ya  kuwahimiza kuandika  barua za madai (CHF) ili kuboresha huduma za kwenye vituo vya afya.

IMEANDALIWA NA;

AMINA PILLY;

AFISA HABARI MANISPAA YA SONGEA.

13 Januari 2021

 

 

 

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa