KATIBU Mtendaji wa Chama cha Waandishi wa Habari mkoa wa Ruvuma(RPC) Andrew Chatwanga amemuomba Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Christina Mndeme kuikumbusha Ofisi ya Waziri Mkuu ahadi ya shilingi milioni 10 kwa ajili ya kuchangia kufungua kituo cha redio.
Chatwanga amesema,Waziri Mstaafu wa awamu ya nne Mizengo Pinda akiwa katika ziara mkoani Ruvuma aliahidi kuchangia kiasi hicho cha pesa kwa ajili ya uanzishwaji wa Redio ya RPC.
Hata hivyo Chatwanga amezitaja ameeleza moja ya mafanikio ambayo chama kimeweza kufanikiwa kuwa na ofisi zake ambazo chama kimepanga katika jengo la Hanga vilevile chama kimeweza kuwaunganisha Waandishi wa Habari na hivyo kuweza kufanya kazi zao kwa Amani.
“kutokuwa na chanzo cha uhakika cha mapato kunasababisha kila mara kupata wakati mgumu kutafuta fedha kwa wadau mbalimbali ikiwemo ofisi yako ili kulipa pango la ofisi”,alisema Chatwanga.
Chama cha waandishi wa Habari mkoa wa Ruvuma ni umoja uliosajiliwa kisheria na kinaendesha shughuli zake kwa kufuata sheria, Kanuni na taratibu za nchi hadi sasa kina wanachama Zaidi ya 45 lakini wanachama 38 pekee ndio wapo hai.
Imeandikwa na
Victoria Ndejembi
Kitengo TEHAMA Manispaa Songea
Agosti 11,2018.
SONGEA MUNICIPAL COUNCIL
Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA
Simu ya Mezani: 025 2602970
Simu ya Kiganjani:
Barua Pepe: info@songeamc.go.tz
Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa