• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

SERIKALI kumaliza kero ya maji Nyasa

Tarehe ya kuwekwa: October 29th, 2018

WAZIRI wa maji Profesa Makame Mbarawa amesema Serikali itahakikisha miradi yote ya maji vijijini na mijini inakamilika kwa wakati ili kuwaondolea kero ya maji Safi na Salama wananchi  ili waweze kufanya kazi kwa bidii za kujiletea maendeleo.

Aliyasema hayo hivi karibuni alipofanya ziara ya siku mbili ya kukagua miradi ya maji katika  katika kijiji cha Ukuli Kata ya kingerikiti na kata ya Tingi.

Profesa Mbarawa alifafanua kuwa aliamua kufanya ziara ya kukagua miradi hiyo ya maji ili aione kwa macho na siyo kusubiri kuletewa kwa maandishi ili azijue  changamoto gani zilizopo katika miradi hiyo ili aweze kuitatua na kuhakikisha Wananchi wanapata maji safi na Salama ikiwa ndilo lengo kuu la Serikali.

Aliongeza kuwa kwa muda mrefu alisikia kuna tatizo la maji katika kata ya Tingi na Kingerikiti hivyo akaamua aje aone,na kutolea ufafanuzi wa kuwa katika mradi wa Ukuli  kuna tatizo la kupasuka kwa viungio vya kwenye bomba kutokana na bomba kupita kwenye miteremko mikali ikitokea kijiji cha burma na kuvuka hadi kijiji cha Ukuli na akasema ameona na ameliona tatizo ambalo atatuma wataalam kutoka Wizara yake ili waweze kutatua tatizo hilo na maji yaweze kutoka na wananchi wafurahie huduma ya maji safi na salama  kwa kuwa  serikali ilishatoa tsh 1,129,433,944.00.kwa ajili ya kutekeleza mradi wa Ukuli-Kingerikiti.

 

“nimefanya ziara ya siku mbili kuja katika kijiji hiki kwa lengo la kutatua tatizo lilopo katika eneo hili badala ya kukaa ofisini na kusubiri kuletewa tatizo kwa maandishi lakini leo nimefurahi nimekagua na niko huku kwenye hii miteremko ambayo nimefanikiwa kuona tatizo lililopo na nitatuma wataalam kuja kurekebisha bomba viungio hivi ambavyo vinapasuka tujue tatizo kubwa ni nini kwa kutumia fedha kidogo na kwa haraka tuweze kutatua tatizo lililopo na hatimaye wanachi waweze kupata maji safi na salama kwa kuwa mapendekezo niliyopata awali ni kupitisha mabomba haya sehemu nyingine”

Wakazi wa kijiji cha Ukuli kata yakingerikiti wakiongelea tatizo la maji katika kijiji hicho wanatumia umbali mrefu wa kilomita tatu hadi tano kutafuta huduma  ya maji hivyo serikali ikifaulu kukamilisha mradi huo itakuwa imewapunguzia kero nzito ya upatikanaji wa maji katika eneo hilo.

Awali akitoa taarifa ya kero ya maji katika eneo hilo kwa Waziri wa maji  kwa niaba ya wananchi wa kata ya Kingerikiti Diwani wa kata ya Kingerikiti Alto Komba ambaye pia ni mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa alisema Tatizo hilo ni kubwa linalowafanya wananchi kutembea umbali mrefu kutafuta huduma ya maji safi na salama.

Aidha alitumia fursa hiyo kuziagiza Halmashauri Nchini  kusimamia vizuri miradi ya maji kuanzia kutangaza zabuni na kuwateua wakandarasi wenye sifa na uwezo wa kifedha ili waweze kukamilisha miradi kwa wakati na kutanguliza maslahi ya wanachi bila kujali maslahi yao binafsi.

Katika kijiji cha Tingi alikagua mradi wa maji wenye thamani ya tsh 361,233,107/= na kuwataka wanachi kuwa na subira wakati mradi huo unakamilishwa na kuwaahidi Serikali itahakikisha inachukua hatua ya kuwaleta wataalam na kuongeza chanzo kingine cha maji ili upatikanaji wa maji safi na salama uwe asilimia 85 kwa vijijini na mjini iwa aslimia 90 ifikapo mwaka 2020.

Aidha Waziri Mbarawa alitoa wito kwa jamii ya watanzania kuvilinda na kuvitunza vyanzo vya maji kwa kuacha kulima kwenye vyanzo vya maji na kuacha kukata miti ovyo ili maliasili iliyopo kwenye vyanzo vya maji viendelee kutoa maji kwa wakazi wa maeneo yote nchini.

Miradi hiyo ya maji itahudumia watu 6286 kwa kata ya kingerikiti na watu 7326 kwa kata ya tingi kwa mujibu wa sensa ya watu na makazi ya mwaka 2012.

IMEANDALIWA NA

NETHO C. SICHALI

AFISA HABARI

NYASA DC

0783662568/0767417597

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa