• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

SERIKALI YAJIPANGA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WATUMISHI WA UMMA RUVUMA.

Tarehe ya kuwekwa: July 6th, 2022

Na,

AMINA PILLY,

AFISA HABARI MANISPAA.

6 JULAI 2022

Serikali imejipanga kutatua changamoto mbalimbali zinazowakabili watumishi wa umma Mkoani Ruvuma.

Hayo yamebainishwa na Waziri wa nchi Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi na Utawala bora, Mheshimiwa Jenista Mhagama (Mb) aliyefanya ziara ya kutembelea Halmashauri ya Manispaa ya Songea leo tarehe 6 Julai 2022 kwa lengo la kutambua kero zinazowakabili watumishi wa umma pamoja na kukagua utekelezaji wa mpango wa kunusuru kaya maskini (TASAF).


Akizungumza na watumishi wa Manispaa ya Songea, Mhe. Mhagama amewataka Maafisa rasilimali watu wa Mkoa pamoja na Manispaa ya Songea kuhakikisha wanatatua changamoto mbalimbali zinazowakabili watumishi wa umma kabla ya kuzifikisha Wizarani.

Amewasisitiza Maafisa utumishi hao kutekeleza majukumu yao ikiwemo na kusimamia nidhamu na uwajibikaji wa watumishi wa umma kwa kufuata kanuni na taratibu za utawala bora.

Mhe. Mhagama ametoa rai kwa watumishi wa umma kuhakikisha wanafanya kazi kwa bidii kwa kuzingatia maadili ya utumishi wa umma kwa lengo la kuleta maendeleo kwa wananchi ambapo Serikali imeendelea kuboresha maslahi ya watumishi kwa kuongeza mishahara pamoja na posho za safari kuanzia mwaka mpya wa fedha 2022/2023.

Aliongeza kuwa Serikali imejipanga kuboresha mfumo wa ajira nchini ambapo kwa mwaka wa fedha 2022/2023 ajira mpya elfu thelathini zinatarajiwa kutolewa pamoja na kupandisha vyeo na madaraja kwa watumishi zaidi ya Laki moja pia, watumishi elfu nane na themanini waliokidhi vigezo watabadilishwa vyeo.

Akizungumza kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma, Pololet Kamando Mgema Mkuu wa Wilaya ya Songea amewataka watumishi wa umma kutimiza wajibu wao kwa kuongeza ufanisi katika utendaji kazi pamoja na kuunga mkono jitihada za Serikali ya Awamu ya 6 za kuleta maendeleo nchini.

Pololet alisema kuwa Mkoa wa Ruvuma una upungufu wa watumishi elfu 80238 katika idara mbalimbali ambapo hadi sasa jumla ya watumishi wa umma walioajiriwa katika ofisi ya Mkoa ni elfu kumi na tatu.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Manispaa ya Songea Dkt. Frederick Sagamiko alisema kuwa Manispaa ya Songea imetekeleza shughuli mbalimbali kwa mujibu wa muongozo wa utumishi wa umma kwa kusimamia zoezi la upandishaji madaraja kwa watumishi pamoja na kubadilisha vyeo (muundo)  kwa watumishi 92 waliojiendeleza.

Akibainisha utekelezaji wa mpango wa kunusuru kaya maskini (TASAF) kwa Manispaa ya Songea, Dkt Sagamiko alisema kuwa katika kipindi cha Julai 2021 hadi Juni 2022 Manispaa ya Songea ilipokea jumla ya shilingi Bilioni 1.3 kwa ajili ya kuwezesha utekelezaji wa mpango wa kunusuru kaya maskini kwa awamu ya pili ambapo jumla ya kaya elfu 5639 zinanufaika na mpango huo.

Mwisho.

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa