• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Songea MC Yadhamiria Kuboresha Lishe na Kuondoa Udumavu

Tarehe ya kuwekwa: July 25th, 2025

Mkurugenzi wa Manispaa ya Songea  Wakili. Bashir Muhoja, amezitaka idara zote zinazohusika na huduma za jamii kushirikiana kikamilifu na Idara ya Afya kupitia kitengo cha lishe ili kuhakikisha utekelezaji wa masuala ya lishe unafanyika kwa ufanisi zaidi katika jamii.

Akizungumza wakati wa kikao cha tathmini ya utekelezaji wa shughuli za lishe katika manispaa hiyo, Mkurugenzi huyo alisisitiza kuwa elimu ya lishe ni silaha muhimu katika kupunguza changamoto ya watoto kuzaliwa na uzito pungufu wa chini ya kilo 2.5, hali inayochangiwa kwa kiasi kikubwa na mimba za utotoni.

"Idara ya Afya inapaswa kusimamia kwa karibu utekelezaji wa afua za lishe, huku ikishirikiana kwa karibu na idara ya elimu, maendeleo ya jamii, ustawi wa jamii, kilimo na fedha ili kutoa elimu kwa jamii juu ya madhara ya mimba za utotoni na umuhimu wa lishe bora," alisisitiza Mkurugenzi.

Aidha, alielekeza kuwa kila shule ya msingi na sekondari ndani ya Manispaa iwe na bustani ya mboga mboga zitakazohusishwa na vilabu vya lishe kwa lengo la kuwahamasisha watoto kujifunza na kupata lishe bora wakiwa shuleni.


Kwa upande wake, Afisa Lishe wa Manispaa hiyo, Bw. Robert Sinkamba, alisema kuwa uanzishaji wa vilabu vya lishe unaendelea kwa mafanikio makubwa, ambapo hadi sasa vilabu hivyo vimeanzishwa katika shule  za msingi na sekondari kwa 72% wanafunzi kupata chakula shuleni.

“Tumekuwa tukitumia njia ya uhamasishaji kuanzisha vilabu vya lishe mashuleni, na zoezi hili limefanyika kwa mafanikio makubwa. Vilabu hivi si tu vinaelimisha kuhusu lishe, bali pia vimekuwa kichocheo kikubwa cha uzalishaji wa bustani za mboga,” alisema Simkamba.

Naye Kaimu Mweka Hazina wa Manispaa ya Songea, Elliassa Urrasa, alisema kuwa kwa mwaka wa fedha 2024/2025 Manispaa hiyo imetumia asilimia 100 ya bajeti iliyotengwa kwa ajili ya lishe. Aliongeza kuwa kwa mwaka wa fedha 2025/2026, Manispaa imetenga kiasi cha shilingi milioni 80 kwa ajili ya kuendeleza na kuimarisha shughuli za lishe katika jamii.

Mikakati hii inalenga kuhakikisha kuwa jamii ya Songea inakuwa na uelewa sahihi kuhusu lishe bora na umuhimu wake katika afya ya watoto, pamoja na kupunguza athari za mimba za utotoni zinazoathiri ukuaji na afya ya watoto wachanga

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA July 08, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 July 04, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • Dkt. Samia Awasili Ruvuma.

    July 30, 2025
  • Mhe. Jenista Waziri wa Afya; Serikali yapambana kupunguza Maambukizi Mapya ya Virus vya Homa ya INI.

    July 29, 2025
  • Songea MC Yadhamiria Kuboresha Lishe na Kuondoa Udumavu

    July 25, 2025
  • Songea MC - Yaibuka na Ushindi katika Mechi ya Kirafiki Dhidi ya Namtumbo.

    July 24, 2025
  • Tazama zote

Video

Dkt. Samia Akiwasili Songea
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa