• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

TAARIFA YA UTARATIBU WA MATUMIZI YA STENDI KUU YA TANGA NA STENDI YA MFARANYAKI.

Tarehe ya kuwekwa: October 1st, 2021

NA,

AMINA PILLY,

AFISA HABARI MANISPAA.

01.10.2021

“Stendi ya Mfaranyaki iendelee kutumika kwa ajili ya matumizi ya daladala zinazosafirisha abiria tu ndani ya Manispaa ya Songea”

Hayo yamebainishwa na Mkuu wa Wilaya ya Songea Pololet Kamando Mgema hapo jana tarehe 30 Septemba 2021 wakati akiwasilisha makubaliano ya kikao kilichofanyika tarehe 29 Septemba 2021 kati ya Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Generali Wilbert Ibuge, viongozi wa Halmashauri ya Manispaa ya Songea pamoja na viongozi wa umoja wa wasafirishaji abiria Ruvuma (UWARU).

Mgema alieleza kuwa kila mmiliki/ kampuni ya mabasi ya usafirishaji anatakiwa kuhakikisha ifikapo tarehe 30 Desemba 2021 iwe imehamishia shughuli zake za kukatia tiketi na mizigo katika stendi kuu ya Tanga na ofisi hizo ziwe zimehamishwa katika stendi ya Mfaranyaki.

Aliongeza kuwa mabasi yote ya Mikoani yakifika na abiria katika stendi kuu ya Tanga kuanzia muda wa saa 4:00 usiku, na endapo katika stendi hiyo hakuna daladala ya kuwasafirishia abiria kwa ajili ya kuwaleta katikati ya Mji, Mabasi  yameruhusiwa kuwaleta abiria katika stendi ya Mfaranyaki na utaratibu huu ni kwa muda wa mpito wa miezi mitatu kuanzia tarehe 30 Oktoba hadi tarehe 30 Desemba 2021.

Mabasi yote ya abiria yanapoelekea stendi ya Tanga nyakati za asubuhi yameruhusiwa kuchukua abiria wenye tiketi katika stendi ya Mfaranyaki kuanzia muda wa saa 10:00 hadi 10:30 alfajiri na yanapoelekea stendi kuu ya Tanga yanaruhuwiwa kuchukua abiria kituo cha Bombambili, Msamala na mshangano, na ifikapo saa 10:31 Alfajiri mabasi yote hayaruhusiwi kuwepo katika stendi ya Mfaranyaki. “Mgema Alisisitiza”

Alihitimisha kwa kusema kuwa mabasi yote yanayofanya safari zake kupitia barabara ya Lindi yataanza safari zake stendi kuu ya Tanga na yanaporudi yatashusha abiria katika kituo cha Seedfarm, endapo yatafika kuanzia saa 4:00 usiku na katika basi hilo kuna abiria wanaokwenda maeneo ya Bombambili, Msamala na Mshangano basi hilo litalazimika kumalizia safari yake katika stendi kuu ya Tanga.

 

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • MWENGE WA UHURU WAPOKELEWA MKOANI RUVUMA

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma Awapongeza Wastaafu 86 wa Kada ya Ualimu Mkoani Ruvuma

    May 08, 2025
  • Kamati ya Siasa Wilaya Yaridhishwa na Hatua za Miradi ya Maendeleo

    May 06, 2025
  • Tazama zote

Video

YALIYOJIRI MAKABIDHIANO YA MBIO ZA MWENGE WA UHURU
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa