• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

Tarehe ya kuwekwa: May 30th, 2025

Mamlaka ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) Mkoa wa Ruvuma imefanikiwa kufuatilia na kuhakikisha kurejeshwa kwa kiasi cha Shilingi Milioni 9.2 za mapato ya ndani zilizokusanywa kupitia mfumo wa kielektroniki na mawakala wa halmashauri lakini hazikuwasilishwa benki kama inavyotakiwa kisheria.

Akizungumza na vyombo vya habari, Naibu Mkuu wa TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma, Bi. Janeth Haule, alisema kuwa hatua hiyo ni sehemu ya juhudi za kuhakikisha nidhamu ya kifedha na uwajibikaji katika taasisi za umma.


Ufuatiliaji huo umechangia kuongezeka kwa makusanyo katika Halmashauri ya Wilaya ya Songea, ambapo makusanyo kupitia mfumo wa kielektroniki yamepanda kutoka asilimia 50 hadi asilimia 102 kwenye sekta za kilimo, mifugo na uvuvi, biashara, ardhi na maliasili.

Aidha, TAKUKURU imetoa ushauri wa kiufundi kuhusu marekebisho ya miradi mitatu yenye thamani ya Shilingi Bilioni 29.9 inayohusisha sekta za miundombinu, kilimo, na fedha, ili kuziba mianya ya rushwa.

Katika kipindi cha Januari hadi Machi 2025, TAKUKURU Ruvuma imefanya chambuzi tatu, warsha tatu, na kufanikisha maazimio 16 ya kuziba mianya ya rushwa. Pia, taasisi hiyo imeendesha semina 24, kuimarisha klabu 53 za kupinga rushwa, mikutano ya hadhara 26, maonesho sita, makala mbili, na vipindi vitatu vya redio.

Programu za uelimishaji zimefanyika katika kata 12, ambako jumla ya kero 118 ziliibuliwa,  kati ya hizo, 89 tayari zimetatuliwa na 29 zinaendelea kufanyiwa kazi.

Kwa upande wa malalamiko, TAKUKURU ilipokea jumla ya malalamiko 100, ambapo 80 yalihusu rushwa na 20 hayakuhusu rushwa. Kesi nne zilifikishwa mahakamani na hadi sasa tatu zimeamuliwa kwa ushindi wa Jamhuri.

Bi. Haule ametoa wito kwa wananchi kujiandaa na kushiriki kikamilifu katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025, kwa kuepuka vitendo vya rushwa ili kuwachagua viongozi waadilifu watakaolinda maslahi ya umma na kuleta maendeleo endelevu.

Mwisho

AMINA PILLY

KITENGO CHA MAWASILIANO SERIKALINI

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa