• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

TAKUKURU Ruvuma iilivyookoa sh.milioni 43 toka kwa Kampuni za uchimbaji madini

Tarehe ya kuwekwa: October 16th, 2019

TAASISI ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa TAKUKURU mkoani Ruvuma imeokoa zaidi shilingi milioni 43  kutoka Kampuni zinazochimba makaa yam awe katika eneo la Ngaka wilayani Mbinga Mkoani Ruvuma.

Akitoa taarifa kwa wanahabari katika kipindi cha utendaji kazi cha TAKUKURU mkoani Ruvuma kuanzia Julai hadi Septemba 2019,Mkuu wa TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yustina Chagaka,amesema fedha hizo zimeweza kulipwa katika Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga kama ushuru wa huduma.

Chagaka amesema TAKUKURU ilifanya uchunguzi na kubaini kuwa Kampuni hizo zilikuwa hazilipi ushuru wa huduma kwa miaka mingi na kwamba baada ya kubaini hali hiyo ilitoa ushauri kwa mamlaka husika hali hali iliyosababisha Kampuni hizo kuanza kulipa ushuru.

“Fedha hizo zimelipwa ndani ya mwezi Septemba,TAKUKURU katika kipindi hiki imefanya uchambuzi wa mifumo ili kubaini mianya ya rushwa katika ukusanyaji wa mapato katika Halmashauri za wilaya ya Mbinga,Nyasa,Namtumbo na Tunduru’’,anasema Chagaka.

Kwa mujibu wa Mkuu huyo wa TAKUKURU,katika kipindi hicho TAKUKURU ukusanyaji wa kodi kwa kutumia mashine za kielekroniki na kufuatiliaji utoaji wa stakabadhi katika maduka 39 katika Wilaya za Songea,Mbinga,Namtumbo na Tunduru ili kuona iwapo wafanyabiashara wanatoa stakabadhi kwa wateja wao na kama wateja wanaomba stakabadhi baada ya kununua bidhaa.

Hata hivyo amesema katika utafiti huo imebainika kuwa ni asilimia 50 tu ya wenye maduka ndiyo wanatoa risiti na asilimia 50 ya wananchi wanaomba stakabadhi baada ya kununua bidhaa na kusisitiza kuwa elimu inatakiwa kuwa endelevu kwa jamii kuhusu umhimu wa stakadhi baada ya kununua bidhaa.

Chagaka amesema TAKUKURU katika kipindi cha kuanzia Julai hadi Septemba 2019 ilipokea taarifa 93 kutoka kwa wananchi na amezitaja Taasisi zilizoongoza kwa kulalamikiwa kuwa ni  serikali za vijiji na mitaa taarifa 22,Polisi 15,Ardhi 14,Halmashauri saba,Elimu tano na midini taarifa mbili.

Kulingana na Chagaka katika kipindi hicho TAKUKURU imefuatilia miradi ya maendeleo 10 ili kujiridhisha iwapo fedha zilizotengwa kwa ajili ya utekelezaji zimetumika kama ilivyokusudiwa.

Amesema miradi hiyo ipo katika sekta za Ujenzi na Miundombinu,Afya,maji na Barabara yenye thamani ya zaidi ya shilingi bilioni tano na kwamba TAKUKURU pia imefuatilia fedha za ruzuku ya elimu zinazotolewa kwa ajili ya uendeshaji wa shule.

”Ufuatiliaji huo umefanyika katika shule za msingi 40 katika kipindi cha  Januri hadi Juni 2019,kiasi cha shilingi 98,912,306.02 zimefuatiliwa matumizi yake’’,alisema.

TAKUKURU ni chombo kilichopewa dhamana kwa mujibu wa Sheria ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa namba 11 ya mwaka 2007 ya kuongoza vita dhidi ya rushwa na ufisadi.

Imeandikwa na Albano Midelo

Afisa Habari Manispaa ya Songea

Oktoba 16,2019

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa