• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

TALGWU RUVUMA YAPATA VIONGOZI WAPYA.

Tarehe ya kuwekwa: April 22nd, 2021

Katibu wa Chama cha Wafanyakazi wa Serikali za Mitaa Tanzania ‘TALGWU ‘ Ashiraff Chussi ameendesha zoezi la uchaguzi wa Matawi 6 yenye jumla ya wanachama 558 katika Halmashauri ya Manispaa ya Songea hapo jana 21 aprili 2021 uliofanyika kwa nyakati tofauti katika ukumbi wa Ushirika Songea Mjini.

Chussi alisema Chama cha TALGWU kinafanya kazi kwa mujibu wa katiba  toleo la mwaka 1995  ambacho kiliundwa chini ya sheria ya vyama vya wafanyakazi NA.10 Ya mwaka 1998.

Alisema kuwa  kwa mujibu wa katiba ya chama hicho imewataka kufanya uchaguzi wa matawi, Mkoa  kila baada ya miaka 5 mitano kwa lengo la kuwapata viongozi wapya ambao watakuwa wanasimamia na kutatua kero zinazowakabili  wanachama wa chama hicho.

 Chama hicho chenye muundo wa uongozi kuanzia ngazi ya chini ( matawini, Wilaya, Mkoa na Taifa) ambapo kabla ya kuendesha taratibu za uchaguzi huo, Chama hicho hutangaza nafasi mbalimbali za uongozi ambazo hugombewa na wagombea  ambao ni watumishi wanachama wa TALGWU ikizingatiwa   sheria na kanuni zilizowekwa.

Katika kutekeleza hilo chama cha TALGWU  Mkoa wa Ruvuma kimekamilisha kusimamia mwenendo mzima wa uchaguzi katika Halmashauri ya Manispaa ya Songea  ambapo kimefanikiwa kuwapata viongozi wapya wa matawi kwa nafasi mbalimbali  za uongozi wa mwenyekiti, katibu na wajumbe wake.

Aliongeza kuwa  uchaguzi huo unaendelea kufanyika  kwa kila Halmashauri zote 8 nane zilizopo Mkoani Ruvuma na baada ya kukamilika kwa matawi yote kutafanyika  uchaguzi ngazi ya Mkoa ambao unatarajia kufanyika kuanzia mwezi julai 2021.

 Akibainisha majukumu ya viongozi hao waliochaguliwa kwa mujibu wa katiba ya TALGWU  ambayo inawataka kufanya kazi kwa weredi ikiwemo na kutetea haki za wafanyakazi, kuboresha na kuendeleza hali nzuri za wanachama wakiwa kazini, kutoa elimu kwa wanachama kuhusu  nidhamu kwa watumishi mahala pa kazi na kuondoa migogoro kati ya mwajiri na mwanachama. “ Chussi alisisitiza”.

Amewataka wanachama wa TALGWU Mkoani Ruvuma kujitokeza kwa wingi wakati zinapotangazwa nafasi mbalimbali za uongozi kupitia  Chama cha TALGWU kuanzia ngazi ya Matawi  ili kujijengea uwezo na kujiamini  na kumwezesha mwanachama kuwa na sifa za  kugombea nafasi mbalimbali ngazi ya juu( Mkoa na Taifa ).

Amewatoa hofu wanachama wa TALGWU juu ya upatikanaji wa t-shirt za Mei Mos kuwa ofisi yake tayari imeshapokea t-shirt  ambazo zitagawiwa mara baada ya taratibu za kiofisi kukamilika.

Mei Mos  mwaka 2021 itafanyika kimkoa  Wilayani  Nyasa.

IMEANDALIWA NA,

AMINA PILLY,

AFISA HABARI MANISPAA YA SONGEA.

22.04.2021

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • MWENGE WA UHURU WAPOKELEWA MKOANI RUVUMA

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma Awapongeza Wastaafu 86 wa Kada ya Ualimu Mkoani Ruvuma

    May 08, 2025
  • Kamati ya Siasa Wilaya Yaridhishwa na Hatua za Miradi ya Maendeleo

    May 06, 2025
  • Tazama zote

Video

YALIYOJIRI MAKABIDHIANO YA MBIO ZA MWENGE WA UHURU
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa