• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

TANGAZO TANGAZO TANGAZO

Tarehe ya kuwekwa: June 16th, 2020

TUME YA TAIFA YA UCHAGUZI

 UWEKAJI WAZI DAFTARI LA AWALI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA 


AFISA MWANDIKISHAJI JIMBO LA SONGEA MJINI ANAWATANGAZIA WANANCHI WOTE WA HALMASHAURI YA MANISPAA SONGEA KUWA, ITAWEKA WAZI DAFTARI LA AWALI LA WAPIGA KURA KWA SIKU NNE KUANZIA TAREHE 17 HADI 20 JUNI MWAKA 2020.

UWEKAJI WA DAFTARI UTAFANYIKA KWENYE VITUO VYOTE VILIVYOTUMIKA KWENYE UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA NA UTAZINGATIA TAHADHARI ZOTE ZA KIAFYA KUHUSU KUZUIA MAAMBUKIZI YA UGONJWA WA COVID- 19 UNAOSABABISHWA NA VIRUSI VYA CORONA.

UWEKAJI WAZI UTAWAHUSISHA WAPIGA KURA WALIOJIANDIKISHA KWENYE DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA MWAKA 2015 NA WALE WALIOJIANDIKISHA WAKATI WA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA AWAMU YA KWANZA MWEZI JANUARI, 2020 NA MWEZI MEI 2020 LAKINI HAWAKUHAKIKI TAARIFA ZAO WAKATI WA UWEKAJI WAZI DAFTARI LA AWALI LA WAPIGA KURA.

MPIGA KURA ANAWEZA KUHAKIKI TAARIFA ZA MPIGA KURA:-

MPIGA KURA ATAFIKA KITUO ALICHOJIANDIKISHA NA KUHAKIKI TAARIFA ZAKE KWENYE ORODHA ITAKAYOBANDIKWA KATIKA KITUO HICHO.

KUPITIA SIMU YA KIGANJANI KWA KUPIGA NAMBA *152*00# NA KUFUATA MAELEKEZO.

MPIGA KURA ATAPIGA SIMU NAMBA 0800112100 NA KUFUATA MAELEKEZO YATAYOMUUNGANISHA NA MTOA HUDUMA.AU KUPITIA TOVUTI YA TUME www.nec.go.tz NA KUBOFYA SEHEMU ILIYOANDIKWA UHAKIKI.

MAMBO YA KUZINGATIA WAKATI WA UHAKIKI

IWAPO MPIGA KURA AMEHAKIKI TAARIFA NA KUTAKA KUFANYA MAREKEBISHO, ATATAKIWA KWENDA SHULE YA MSINGI MFARANYAKI ILIYOPO KARIBU NA MSIKITI WA WILAYA SONGEA MJINI KUREKEBISHA TAARIFA ZAKE.

MPIGA KURA ANAYETAKA KUMUWEKEA PINGAMIZI MPIGA KURA ASIYE NA SIFA, ATAKWENDA KWENYE KITUO CHA SHULE YA MSINGI MFARANYAKI.

WAPIGA KURA WANATAKIWA KUTOA TAARIFA ZA NDUGU WALIOFARIKI ILI WAONDOLEWE KWENYE DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA.

IWAPO MPIGA KURA ATAHAKIKI TAARIFA ZAKE NA KUBAINI KUWA PICHA YAKE HAIPO, ATATAKIWA KWENDA KWENYE KITUO CHA SHULE YA MSINGI MFARANYAKI ILI APIGWE PICHA NYINGINE.

UWEKAJI WAZI WA DAFTARI LA AWALI LA WAPIGA KURA HAUTAHUSIKA KUANDIKISHA WAPIGA KURA WAPYA AU KUHAMISHA TAARIFA ZA WAPIGA KURA WALIOHAMA KATA AU JIMBO.

EWE MWANANCHI

KUMBUKA KUZINGATIA KANUNI ZA AFYA KWA KUFUATA MAELEKEZO UTAKAYOPEWA KITUONI ILI KUJIEPUSHA NA MAAMBUKIZI YA VIRUSI VYA CORONA.

TANGAZO HILI LIMETOLEWA NA ;

AFISA MWANDIKISHAJI

JIMBO LA SONGEA MJINI

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • MWENGE WA UHURU WAPOKELEWA MKOANI RUVUMA

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma Awapongeza Wastaafu 86 wa Kada ya Ualimu Mkoani Ruvuma

    May 08, 2025
  • Kamati ya Siasa Wilaya Yaridhishwa na Hatua za Miradi ya Maendeleo

    May 06, 2025
  • Tazama zote

Video

YALIYOJIRI MAKABIDHIANO YA MBIO ZA MWENGE WA UHURU
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa