• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

TASAF KIPINDI CHA PILI AWAMU YA TATU MANISPAA YA SONGEA YAANZA NA UHAKIKI WA KAYA.

Tarehe ya kuwekwa: June 30th, 2020

Uwajibikaji na uadilifu kwa wataalamu ni muhimu katika kusimamia zoezi la uhakiki wa Walengwa wa kaya maskini TASAF ambao  utasaidia kupata Takwimu sahihi  za wanufaika Halisi  ndani ya Manispaa ya Songea.

Kauli hiyo imetolewa na Mwakilishi wa Mkurugenzi Mtendaji TASAF Daniel Makinda katika mafunzo ya wakuu wa Idara na Vitengo yanayohusu Utekelezaji wa kipindi cha pili cha awamu ya tatu TASAF yanayoendelea kufanyika katika ukumbi wa Manispaa ya Songea kuanzia 29-30/06/2020.

Makinda alisema, Lengo kuu la mafunzo haya ni kuwajengea uwezo wa kiutendaji katika kusimamia Uhakiki wa kaya maskini utakaofanyika mara baada ya mafunzo hayo ili kupata Takwimu HALISI za  Walengwa HALISI ambao wamefariki (ambao walikuwa ni kaya ya mtu mmoja asiye na mtegemezi, kaya ambayo imehama, kaya ya Kiongozi wa Kijiji, kaya ya mjumbe wa Kamati ya Usimamizi ya Jamii (CMC), kaya ambayo haikufika kuchukua malipo yake  mara mbili mfululizo. Takwimu hizo zitakusanywa kwa njia ya DODOSO, na kuingizwa kwenye Mfumo wa Takwimu.

Alisema “Manispaa ya Songea ina wanufaika TASAF  4822, kwa mitaa 53 katika kata 21 zilizopo manispaa ya  Songea ambazo zinapata huduma ya TASAF. Aliongeza kuwa Utekelezaji wa Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini pia umewezesha kaya za walengwa kujikita kwenye shughuli za kukuza kipato na kujiimarisha kiuchumi ikiwemo ufugaji, uvuvi, kilimo na biashara ndogo ndogo.

 Aliongeza kuwa, zipo baadhi ya kaya za  wananchi wanaoishi katika hali duni kwenye maeneo ambayo hayakufikiwa, Hivyo Kipindi cha Pili katika Awamu ya Tatu ya TASAF  kaya zote zinazoishi katika mazingira duni zipate usaidizi wa Serikali kupitia TASAF kwa kuwawezesha kufanya kazi na kupambana na umaskini.”

 Aliongeza kuwa, Mkazo mkubwa katika Kipindi cha Pili utawekwa katika kuwezesha Kaya zitakazoandikishwa kwenye Mpango kufanya kazi ili kuongeza kipato na kuhakikisha kwamba huduma za jamii zinaongezwa na kuboreshwa  na kuendeleza rasilimali watoto hususani katika upatikanaji wa elimu na afya. 

 Aliwasisitiza  Viongozi hao kufanya kazi kwa uadilifu na weredi wakati wa utekelezaji wa Zoezi hili  kama maagizo yaliivyotolewa na Mh Rais katika hotuba  yake wakati wa uzinduzi wa Kipindi cha Pili kuhusu uwepo wa kaya hewa. “Nanukuu. “ Uwepo wa kaya hewa katika maeneo ya utekelezaji ni aibu sana kwa viongozi wa Mikoa, Wilaya na Halmashauri. Nitoe wito kwa wahusika wote kusimamia vizuri mradi huu. Serikali haitakuwa na huruma kwa mtu yeyote. Kufanikiwa ama kutofanikiwa kwenye maeneo yenu itakuwa mojawapo ya vipimo nitakavyotumia kujua kama mnastahili kuendelea na nafasi mlizonazo au la. Siwatishi lakini huo ndio ukweli” mwisho wa kunukuu.

Mwisho aliwakumbusha wananchi wote kuchukua tahadhari ya ugonjwa hatari wa COVID-19  ili   kuepuka Mikusanyiko isiyoyalazima, kuvaa barakoa,  kuepuka kushikana  mikono na  kunawa mikono kwa sabuni kwa kutumia maji safi yanayotiririka pamoja na kutumia vitakasa mikono. 

 

IMEANDALIWA NA;

AMINA PILLY,

KAIMU AFISA HABARI-MANISPAA YA SONGEA.

30.06.2020

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa