• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

UGONJWA WA AJABU TISHIO KWA WANAFUNZI

Tarehe ya kuwekwa: September 26th, 2017

UGONJWA WA AJABU TISHIO KWA WANAFUNZI

UGONJWA wa ajabu ambao umezuka katika shule ya msingi Subira iliyopo katika Manispaa ya Songea mkoani Ruvuma tangu Machi mwaka huu bado ni tishio kwa wanafunzi wanaosoma katika shule hiyo.

Mwalimu Mkuu wa shule hiyo Majidu Ngonyani amesema tangu kufunguliwa kwa shule hiyo Septemba 18 mwaka huu hadi jana wanafunzi 45 wameathirika na ugonjwa huo  hali inayoathiri taaluma katika kiwango cha kutisha.

Amesema jana pekee wanafunzi 27 wameanguka na kupoteza fahamu  na kwamba wanafunzi waliokuwa na moyo wa kuhudhuria masomo licha ya kuwepo kwa ugonjwa huo wa ajabu,wameanza kuingiwa na wasiwasi hivyo kuacha kuhudhuria masomo.

Takwimu  za mahudhurio ya wanafunzi za leo Septemba 26 zinaonesha kuwa jumla ya wanafunzi 250 wamehudhuria masomo sawa na asilimia 48 kati ya wanafunzi 539 walioandikishwa katika shule hiyo.

Kwa mujibu wa Mwalimu wa Taaluma wa shule hiyo Sarah Haule,wanafunzi wanaopata ugonjwa huo ni wa kike na kwamba hadi sasa licha ya madaktari kuchukua vipimo kwa wanafunzi wanaugua bado haijafahamika ni ugonjwa gani unaowasumbua.

Mstahiki Meya wa Manispaa ya Songea Alhaji Abdul Hassan Mshaweji na Maafisa wa  Idara ya Elimu Msingi Manispaa hiyo  mara kadhaa wamefanya ziara katika shule hiyo ili kujaribu kutafutia ufumbuzi wa kudumu,hata hivyo hali inazidi kuwa mbaya.

Katika kikao cha Julai 21 mwaka huu,Kamati ya Shule,walimu na wananchi walikubaliana  kufanya maombi maalum yaliyoshirikisha madhehebu mbalimbali ya dini ambayo waliaamini yangeweza kumaliza tatizo.

Kuanzia Alhamis iliyopita hadi Kesho Jumatano Septemba 27,waumini wa dhehebu la SILOAM wanafanya maombi ya siku saba mfululizo katika shule hiyo,hata hivyo bado tatizo linaendelea na kuiacha shule hiyo njia panda.

Mwalimu Mkuu wa shule hiyo amesema licha ya kufanyika maombi yalioshirikisha madhehebu yote,bado tatizo la kuanguka kwa wanafunzi linaendelea ambapo ametahadharisha kuwa kuna hatari ya utoro kuongezeka kwa sababu ya kasi ya kuanguka na kupoteza fahamu idadi kubwa ya wanafunzi.

Mkuu wa Wilaya ya Songea Pololet Mgema ambaye pia ni Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya ya Songea leo amefanya mkutano wa hadhara na wananchi wa Subira katika harakati za kutafutia ufumbuzi wa kudumu tatizo hilo linalowakabili wanafunzi wa kike pekee.

Tatizo lililoikumba shule hiyo limewahi kutokea katika shule ya sekondari Beroya,shule ya msingi Mwengemshindo na Chandarua katika Manispaa ya Songea ambayo ufumbuzi wake ulifanywa kwa maombi maalum ya madhehebu ya dini.

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa