• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

UMOJA WA MATAIFA kuanza kununua mahindi ya Ruvuma

Tarehe ya kuwekwa: July 30th, 2018

SHIRIKA la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Chakula Duniani (WFP) linatarajia kuanza kununua mahindi toka katika Mkoa wa Ruvuma ambao ni miongoni mwa mikoa ambayo ni magwiji wa uzalishaji wa mazao ya chakula.

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amesema ujio wa Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la WFP David Beasley hapa nchini ni fursa itakayowawezesha Watanzania kunufaika kwa kiwango kikubwa katika kilimo, uhifadhi na uuzaji wa mazao ya chakula yanayolimwa hapa nchini.

Waziri Mkuu amesema Tanzania inatarajiwa kuwa na ziada ya chakula msimu wa mavuno utakapokamilika mwaka huu hivyo itahitaji  kupata soko nje ya nchi ili iweze kuuza ziada hiyo.

“Taarifa za Wizara ya Kilimo zinaonesha kuwa mavuno ya mazao ya chakula kama mahindi, maharage na mbaazi yatafikia tani milioni 16 wakati mahitaji ya chakula kwa Watanzania kwa mwaka ni tani milioni 13, hivyo tutakuwa na ziada ya tani milioni tatu,” amesema.

Hatua ya WFP kukubali kununua chakula cha ziada kitakachozalishwa hapa nchini imewahakikishia Watanzania kuwa mazao yao hayatakosa soko.

Mkurugenzi huyo wa WFP ametembelea vijiji kadhaa katika Halmashauri za Songea, Namtumbo na Madaba mkoani Ruvuma amejionea jinsi wananchi walivyopata mavuno mazuri hasa mahindi.

Mkoa wa Ruvuma katika kipindi cha mwaka 2017/2018 umezalisha mahindi tani 933,284.Akitoa taarifa ya NFRA kwa niaba ya Meneja wa Kanda ya Songea Eva Kwavava amesema Mapendekezo ya malengo ya ununuzi kwa mwaka 2018/2019 katika mkoa wa Ruvuma yanaonesha kuwa Halmashauri ya Manispaa ya Songea mgawo ni tani 417 wakati kiasi kilichozalishwa ni tani 58,144,Halmashauri ya Wilaya ya Songea tani 1,983.531,kiasi kilichozalishwa ni tani 227,320 na Halmashauri ya Madaba tani 1,216.466 na kiasi cha tani zilizozalishwa ni 148,408.

Kulingana na mapendekezo hayo Halmashauri ya wilaya ya Mbinga imepangiwa kununua tani 1,189.175,kiasi kilichozalishwa ni tani 165,484,Halmashauri ya Mbinga Mji tani 461.976 na kiasi cha tani zilizozalishwa ni 64,288.

Katika Wilaya ya Namtumbo zitanunuliwa tani 1,068.017,kiasi kilichozalishwa ni tani 134,708,Nyasa tani 663.011 na kiasi kilichozalishwa ni tani 64,432 na wilaya ya Tunduru imezalisha tani 70,500 za mahindi na hakuna wa ununuzi.

Katika msimu wa mwaka 2017/2018 Kanda ya Songea ilipangiwa kununua mahindi tani 6,182,hata hivyo kanda hiyo ilinunua jumla ya tani 11,557,529 baada ya malengo kuongezwa mara mbili.

Kaimu Meneja wa NFRA Kanda ya Songea amesema katika kituo hicho kilichopo Ruhuwiko mjini Songea,kuna tani 21,892.924 za mahindi ambayo yanatokana na ununuzi wa misimu miwili ya 2016/2017 na 2017/2018 na kwamba akiba hiyo ipo katika hali nzuri.

Imeandikwa na Albano Midelo

Afisa Habari Manispaa ya Songea

Julai 30,2018

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • MWENGE WA UHURU WAPOKELEWA MKOANI RUVUMA

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma Awapongeza Wastaafu 86 wa Kada ya Ualimu Mkoani Ruvuma

    May 08, 2025
  • Kamati ya Siasa Wilaya Yaridhishwa na Hatua za Miradi ya Maendeleo

    May 06, 2025
  • Tazama zote

Video

YALIYOJIRI MAKABIDHIANO YA MBIO ZA MWENGE WA UHURU
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa