• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

UNAVYOWEZA kutajirika na miti ya mbao

Tarehe ya kuwekwa: April 10th, 2018

Kilimo cha miti kimepata umaarufu wa ghafla miaka ya hivi karibuni kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo ongezeko la mahitaji ya mazao ya miti.

Wananchi wa mikoa ya kusini ukiwemo mkoa wa Iringa,Njombe na Ruvuma wana fursa kubwa ya kutajirika na miti ya mbao hasa kutokana na hali ya hewa katika mikoa hiyo kuruhusu kustawi vema miti ya mbao ya aina mbalimbali.

Matumizi ya mbao katika kipindi hiki yameongezeka katika kiwango kikubwa kwa sababu miti inatumika kwa mbao, nguzo za umeme, nguzo za kujengea na utengenezeji wa vitu vya thamani .

Hata hivyo Mtaalam wa Shamba la serikali la Misitu  Njombe Godwin Mgunda anasema licha ya kuibuka kwa fursa hii,bado wananchi wengi hawajachangamkia fursa ya upandaji miti ambayo inaweza kubadilisha maisha yao baada ya miaka michache.

“Miti inapofikisha umri wa kuanzia miaka saba huwa tayari kwa kuanza kuvunwa kwa mbao ndogo,hekari moja ya shamba inachukua wastani wa miti 600,wastani wa chini wa mti mmoja kwa sasa uliokomaa ni shilingi 30,000  , inategemea na ukubwa wa mti’’,anasisitiza Mgunda.

Anabainisha kuwa iwapo hekari moja ikiwa na miti iliyokomaa inaweza kuingiza mapato ya shilingi milioni 18 na kwamba anasisitiza kuwa  Kilimo cha miti ni rahisi  kwa sababu ukishapanda hakihitaji uangalizi mkubwa  na wala hauhitajiki uwe karibu na shamba muda wote.

“Mvua inyeshe ama isinyeshe mti wa mbao, ukishachipua huwa haufi kwani huendelea kutumia unyevu wa ardhini. Kazi namba moja unapokuwa umeshakamilisha upandaji wa miti kwenye shamba ni kutengeneza njia za kuzuia moto walau mara moja kwa mwaka, kazi ya pili ni kufyekea miti inapokua walau kwa mwaka mara moja’’,anasema Migunda.

Hata hivyo anasema ardhi ni rasilimali inayopanda thamani kila hivyo ukiwa na shamba la miti,thamani ya ardhi hiyo inazidi kupanda kila siku na miti uliyopanda inazidi kupanda thamani kila siku.

Migunda anazitaja huduma ambazo zinatolewa Shamba la Misitu Njombe(Njombe Forest Plantation) kuwa ni kutoa huduma ya upatikanaji wa mashamba ya kupanda miti ya mbao kwa bei ya kati ya shilingi 200,000 hadi 180,000.

 Huduma nyingine anazitaja kuwa huduma ya kuzalisha ya miche ya miti ya mbao aina ya mikaratusi na pine na kupanda mashambani bei ya shilingi 100 kwa mche,kutoa huduma ya kusimamia shamba kwa mteja aliye mbali na shamba lake na mteja kuunganishwa na serikali kwa ajili ya taratibu za hati.

Imeandaliwa na Albano Midelo

Afisa Habari Serikalini

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa