• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

UTALII wa mikutano kuvutia wengi

Tarehe ya kuwekwa: August 26th, 2018

SERIKALI kupitia Bodi ya Utalii Tanzania (TTB) imeamua kuanzisha kitengo mahususi cha kuvutia utalii wa mikutano kinachojulikana kama 'The National Convention Bureau'.

Kitengo hicho kitakuwa na mamlaka ya kuandaa, kualika na kuvutia mikutano ya kimataifa kufanyika Tanzania.

Mwenyekiti wa TTB, Jaji mstaafu Thomas Mihayo aliwaambia waandishi wa habari mwishoni mwa wiki kuwa chombo hicho kitaanza kama kitengo ndani ya TTB kwa kushirikiana na Kituo cha Kimataifa cha Mikutano Arusha (NICC) ili kufanikisha malengo ya kuvutia utalii wa mikutano na matukio.

"Sekta ya mikutano na matukio (MICE) huzalisha takribani dola za Marekani milioni 300 kwa mwaka, hivyo ni fursa kwa Tanzania kuchangamkia kwani vigezo vyote vya kufanya utalii wa mikutano tunavyo hapa Tanzania," amesema Jaji Mihayo.

Amesema, ushirikiano huu unalenga kuhakikisha shughuli zinazohusu mikutano na matukio zinafanyika kwa utaratibu na utaalamu wa hali ya juu ili kufanikisha soko la utalii wa mikutano na matukio.

Alisema kigezo kikubwa ni kumbi za mikutano, hoteli na usalama ambavyo vyote vinapatikana nchini pamoja na vivutio vya utalii kama mbuga za wanyama na Mlima Kilimanjaro vitakuwa ni sehemu ya kuchochea utalii wa mikutano.

"Mkutano mmoja wa kimataifa huleta watu si chini ya 2000 ambao watahitaji kula, kulala, kufanya matembezi baada ya mkutano hivyo watachochea mzunguko wa fedha na pia watahamasika kutembelea vivutio vya utalii na kupeleka idadi watalii kuongezeka," amesema.

Aliongeza nchi ambazo utalii ni sehemu muhimu ya uchumi kama vile Australia na Malaysia wameanzisha kitengo hicho na kwa Bara la Afrika, nchi ya Rwanda na Afrika Kusini zimeanzisha kitengo hicho na kimewaletea mafanikio kwa kupokea mikutano ya kimataifa nchini mwao.

"Juhudi za makusudi zimechukuliwa na serikali kupitia TTB na AICC kwa kufanya vikao na wadau juu ya uanzishwaji wa kitengo hicho," amesema Jaji Mihayo.

Amesema Bodi ya Utalii imeandaa mafunzo yatakayofanyika mwezi Oktoba kwa wadau kwa lengo la kuhamasisha utalii wa mikutano (MICE) na fursa zinazopatikana kupitia mikutano hiyo.

Wataalamu kutoka nchi za Afrika kusini na Rwanda wanategemewa kuwasilisha mada katika semina hiyo.

Bodi ya Utalii imeendelea kuwa miongoni mwa sekta zinazochangia maendeleo ya uchumi wa Taifa kwa kuchangia asilimia 17.2 ya pato la Taifa zaidi ya asilimia 24 ya mauzo yote ya nje na zaidi ya asilimia 11 ya ajira zote zinazotengenezwa nchini.

CHANZO NI GAZETI LA SERIKALI

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • Bil. 22.9 Kujenga Masoko ya Kisasa Manzese A na B, na Kiwanda cha Kuchakata Mazao ya Nafaka Lilambo

    July 06, 2025
  • MBUNGE SONGEA MJINI AKABIDHI KOMPYUTA NA KUFADHILI UKARABATI WA OFISI ZA POLISI

    June 27, 2025
  • DC Songea bAzindua Dawati la Huduma za Ustawi wa Jamii Stendi ya Mabasi Songea

    June 24, 2025
  • Meya Mbano; Amewataka Wananchi Kulinda Haki za Watoto

    June 16, 2025
  • Tazama zote

Video

Makabidhiano ya Mkataba Soko la Manzese A&B
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa