• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

UTALII WA NDANI;Maajabu ya Jiwe la Mbuji

Tarehe ya kuwekwa: May 10th, 2018

MKOA wa Ruvuma una vivutio vingi tofauti ambavyo bado havitumiki katika kuchangia pato la Taifa na kuinua uchumi wa wananchi wa eneo husika.

Jiwe la Mbuji ambalo lipo katika wilaya ya Mbinga mkoani Ruvuma ni miongoni mwa vivutio adimu na vya kipekee vilivyopo katika Bonde la ziwa Nyasa ambalo linajumuisha mikoa ya Mbeya,Ruvuma na Njombe.

Afisa Maliasili na Utalii wa Mkoa wa Ruvuma Africanus Challe anasema tayari Idara yake imeliingiza jiwe la Mbuji  kwenye orodha ya vivutio vya utalii katika Mkoa wa Ruvuma ili hatimaye kazi ya kutangaza eneo hilo na vivutio vingine iweze kufanyika kwa tija.

Kivutio cha jiwe la Mbuji kimekuwa gumzo kwa wengi waliosikia taarifa za kivutio hicho.Neno Mbuji kwa lugha ya kabila la wamatengo ni "Kitu kikubwa",jiwe hili lipo katika kijiji cha Mbuji kata ya Mbujii na limekuwa kivutio adimu kwa wageni wa ndani na nje ya nchi.

Jiwe la Mbuji lina maajabu mengi yakiwemo jiwe pekee kubwa Mkoani Ruvuma,Lina vyanzo vingi vya maji chini yake,ni vigumu kulipanda bila kuwaona wazee  kwa sababu ni vigumu kupanda na kulizunguka jiwe hilo bila kufuata mila na desturi za kabila la wazee wa kimatengo.

Unapofika katika jiwe hilo inakulazimu kuwatafuta wazee  wanaotoa maelekezo kwa yeyote anayetaka kupanda jiwe hilo,ambalo linaheshimika sana na wakazi wanaolizunguka jiwe hilo.

Utafiti umebaini kuwa,sehemu kubwa ya wananchi wanaolizunguka jiwe jiwe la Mbuji hawajawahi kulipanda wala kulisogelea kwa hofu ya kupoteza maisha.

Mzee Sixmund Ndunguru (90) anasema kuwa ili kupanda jiwe hilo ni lazima uwe na Mwongozaji ambaye ni mzee wa mila ambaye anazifahamu vizuri mila na taratibu za kabila la wamatengo zitakazokuwezesha kupanda jiwe hilo bila matatizo na kufurahia vivutio vilivyopo.

“Ninayafahamu maajabu ya jiwe la Mbuji tangu nikiwa na umri wa miaka mitano,mandhari ya jiwe hili hayajabadilika wala kuharibiwa tangu nilipolifahamu jiwe hili’’,anasema  Ndunguru.

Kulingana na Ndunguru,mimea aina ya matete ambayo imekuwepo katika jiwe hilo tangu miaka ya 1940 alipopanda juu ya jiwe hilo kwa mara ya kwanza akiwa na baba yake mzazi na kwamba kila mtu anaruhusiwa kupanda jiwe hilo kwa kuzingatia maelekezo ya wazee wa mila na desturi.

Serikali ya Kijiji cha Mbuji kwa kushirikina na wazee wa mila wameamua kuboresha mazingira ya eneo la kivutio hicho cha utalii kwa kujenga nyumba za mila za wamatengo,kupika vyakula vya asili na ngoma za jadi ili watalii wakishaona jiwe hilo waweze kupata vyakula na ngoma za asili ya wamatengo hivyo wananchi kujipatia kipato.

Makala hii imeandaliwa na Albano Midelo

Afisa Habari Manispaa ya Songea



Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa