• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

vifahamu vipodozi vinavyotengenezwa na Wajasiliamali wa Manispaa ya Songea.

Tarehe ya kuwekwa: September 25th, 2020

Afisa Biashara Mkoa wa Ruvuma Joseph Kabalo  amesema ili bidhaa ziweze  kukamilika  katika matumizi yake  kwanza zinahitaji  zizalishwe kwa ubora, pia  ili uzalishaji ufanikiwe nilazima bidhaa ziwafikie watumiaji wa mwisho ( final consumer).

Kauli hiyo imetolewa  katika kikao cha wafanyabiashara wazalishaji wa bidhaa za Vipodozi, chaki, na  vifaa vya ujenzi “Gypsum powder”, pamoja na wadau mbalimbali wakiwemo na SIDO, TCCIA, TBS na wafanyabiashara wauzaji wa bidhaa hizo,  kilichofanyika katika ukumbi wa Manispaa ya Songea leo 25.09.2020.

Kabalo alisema lengo la kikao hicho ni kufanya utambulisho wa bidhaa ambazo zinazalishwa Manispaa ya Songea, Mkoani Ruvuma ili kuwaunganisha wafanyabiashara wazalishaji wa bidhhaa za vipodozi, chaki, na vifaa vya ujenzi ambavyo vinazalishwa kwa kutumia malighafi ambazo zinazopatiakana ndani ya Mkoa wa Ruvuma.

Aliongeza kuwa viwanda vinavyoanzishwa na wajasiliamali wenyewe endapo bidhaa zake hazitaweza kutumika ipasavyo vitashindwa kujiendesha kwasababu sisi wenyewe hatutaki kuvitumia, alisema endapo bidhaa hiyo itakuwa haijamfikia mtumiaji wa mwisho,pia  matumizi ya bidhaa hizo yatakuwa hayajakamilika na mfikishaji wa bidhaa hizi kwa watumiaji wa mwisho ni wafanyabiashara waliopo ndani ya Mkoa wa Ruvuma.

Naye Mkurugenzi wa kampuni Power Body Butter George Ndimbo alisema Kampuni hiyo inazalisha bidhaa za vipodozi  vya asili kama vile sabuni ya kuogea, vitakasa mikono, sabuni ya kudekia, sabuni ya kuondoa harufu chooni, mafuta ya kupaka pamoja na rosheni ambazo zina tengenezwa kwa kutumia malighafi zinazolimwa ndani ya Mkoa wa Ruvuma ikiwemo na zao la Mawese ambalo hulimwa Wilaya ya Nyasa.

Ndimbo aliongeza kuwa falsafa ya Tanzania ya viwanda imemsaidia sana kwa kuanzisha kiwanda cha Power Body Butter ambacho licha ya kutengeneza bidhaa hizo, wanakazi nyingine ya kutoa elimu ya afya ya ngozi ili mteja anapotumia bidhaa hizo ngozi yake iwe na muonekano wa kuvutia.

Alibainisha kuwa Power Body Butter yenye makao makuu Mjini Songea kata ya Msamala  inazalisha vipodozi vya asili ambavyo vimetengenezwa kwa kiwango chenye  ubora na vimethibitishwa na TBS.

Naye Afisa uendeshaji biashara SIDO Ruvuma  Linus Kimoro alisema shirika la SIDO linatoa huduma kwa jamii ikiwemo wajasiliamali kwa kuwapatia elimu ya ujasiliamali, kutoa mikopo kwa wajasiliamali, pamoja na kutoa maonesho mbalimbali kwa  wajasiliamali.

Naye Afisa biashara Manispaa ya Songea Furaha Mwangakala alisema baada ya kikao hiki cha wafanyabiashara anategemea kuziona bidhaa hizi za vipodozi, chaki na bidhaa za ujenzi zinauzwa kwenye maduka yetu  ndani ya Mkoa wa Ruvuma ili uzalishaji uweze kuboreka Zaidi.

IMETAYARISHWA NA;

AMINA PILLY;

AFISA HABARI MANISPAA YA SONGEA.

24.09.2020.

  

 

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa