• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

VIJANA 42 wapata mafunzo ya wawezeshaji rika Manispaa ya Songea

Tarehe ya kuwekwa: May 17th, 2018

MANISPAA ya Songea mkoani Ruvuma imeendesha mafunzo ya siku mbili kwa wawezeshaji rika  ngazi ya Kata ambapo jumla ya washiriki 42 wamepata mafunzo hayo.

Akisoma taarifa fupi ya mafunzo hayo yaliyofanyika kwenye ukumbi wa Mkuu wa Wilaya ya Songea,mmoja wa wawezeshaji  rika Mkoa wa Ruvuma Nickson Homange amesema mafunzo hayo yanatolewa kwa siku mbili kila Halmashauri  kwa kufuata mwongozo wa kitaifa wa stadiza maisha.

Hata hivyo amessisitiza kuwa mafunzo hayo yatakuwa yanaendeshwa kwa kutegemea mapato ya ndani ya kila Halmashauri au wilaya na kwamba serikali imeamua kuandaa mafunzo hayo kutokana na changamoto zinazowakumba vijana wengi nchini.

“Vijana wengi wamekata tamaa,lakini hawana stadi za maisha za kukabiliana na changamoto hivyo wanaathirika na mambo mengi ya maisha,kiuchumi,kielimu na magonjwa ya kujamiiana na tabia za kujamiana,matumizi ya dawa za kulevya na matatizo ya uzazi,VVU na UKIMWI’’,anasema Homange.

Mwezeshaji huyo amebainisha Zaidi kuwa,Kutokana na changamoto hizo Wizara imeamua kutoa muongozo ili kuwaandaa wawezeshaji rika wawili kila kata ambao watakuwa na miongozo midogo ya kufanya mafunzo katika jamii.

Ameongeza kuwa mafunzo hayo yatawawezesha vijana kuwa wabunifu kwa kuyatumia mazingira yao kubuni kazi za kufanya ili kujipatia kipato na kuwawezesha vijana kuunda vikundi vya uzalishajimali ili asilimia tano ya mapato ya ndani katika Halmashauri yaweze kuwanufaisha vijana wote.

Mgeni rasmi katika Mafunzo hayo alikuwa ni Katibu wa Mbunge wa Jimbo la Songea mjini Musa Mwakaja ambaye aliwaasa vijana kuwa wasikivu katika mafunzo hayo ili kwenda kutoa habari sahihi kwa vijana wengine ambao watakwenda kuwafundisha katika ngazi ya kata.

Mada zilizofundishwa katika mafunzo hayo ni mzunguko wa maisha ya binadamu,kupevuka na balehe,kuhimili mihemko,mfumo wa uzazi wa binadamu,ngono salama, mawasiliano,mahusiano mema,dawa za kulevya,shughuli za kujipatia kipato,kuepuka mimba za utotoni na uzazi wa mpango.

Imetolewa na Albano Midelo

Afisa Habari Manispaa ya Songea

Mei 17,2018

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa