• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

VIJANA 51 waishio katika mazingira hatarishi wahitimu ufundi VETA Songea

Tarehe ya kuwekwa: September 9th, 2018

VIJANA wanaoshi katika mazingira hatarishi wapatao 51 wamehitimu mafunzo ya kozi fupi katika chuo cha ufundi stadi VETA kilichopo Manispaa ya Songea mkoani Ruvuma.Vijana hao wamefadhiliwa mafunzo hayo kupitia Shrika la PADI kwa ufadhili wa shirika la PACT TANZANIA ambao pia wamewapatia vijana hao vifaa mbalimbali vya kazi kulingana na kozi ambazo wamesomea.

Akisoma risala ya Shirika la PADI kwa niaba ya Mtendaji Mkuu Shirika kilo,Mwakilishi huyo Gift Kilasi amesema ufadhili wa watoto hao ni moja ya miradi ambayo inatekelezwa na USAID kizazi kipya mradi ambao unatekelezwa katika Halmashauri tatu za Wilaya ya Songea ambazo ni Halmashauri ya Wilaya ya Songea,Manispaa ya Songea na Halmashauri ya Madaba.

Kilasi amesema PADI inatekeleza mradi huo tangu Juni 2017 ambapo mradi umelenga kuwafikia walengwa wapatao 35,037 ambao ni watoto wanaoishi katika mazingira hatarishi pamoja na walezi wao ambapo hadi sasa wamefanikiwa kuwafikia walengwa wapatao 31,313 sawa na asilimia 91.

Hata hivyo amesema mradi huo unaendeshwa na wahudumu wa kujitolea wapatao 1017 kwa ajili ya mashauri ya watoto na wahudumu 67 wa kuhudumia vikundi vya kiuchumi na amezitaja huduma ambazo zinatolewa kuwa ni elimu ya malezi na matunzo,elimu ya lishe na tahmini ya hali ya lishe,msaada wa kisaikolojia,ulinzi na usaama wa mtoto,huduma ya afya,elimu na mafunzo ya ufundi stadi,kuboresha hali ya uchumi wa kaya na kuwaunganisha watoa huduma kwa njia ya rufaa.

"Katika kipindi cha mwaka 2018/2019 PADI kwa ufadhili wa PACT TANZANIA limefanikiwa kutoa ufadhili wa mafunzo mbalimbali kwa watoto wanaoshi katika mazingira hatarishi katika chuo cha VETA  ambayo ni kozi za ushonaji.uungaji vyuma,ufundi magari,saluni za kike,mapishi,ufundi bomba,useremala na fani nyingine'',anasisitiza Kilasi.

Mgeni rasmi katika mahafali hayo yaliyofanyika Septemba 8 katika viwanja vya VETA alikuwa ni Mkuu wa wilaya ya Songea pololet Mgema ambaye aliwakilishwa na Katibu Tawala wa Wilaya ya Songea Pendo Ndumbaro ambaye amelipongeza Shirika la PADI kwa kushirikiana na  PACT TANZANIA kufadhili mafunzo hayo ya miezi mitatu kwa watoto wanaoishi katika mazingira hatarishi.

Kupitia Mashirika hayo Vijana hao wametunukiwa vyeti na kupewa vifaa kulingana na kozi walizosomea ambavyo vitawasaidia kujiajiri na kutoa ajira kwa wengine ambao hawakubahatika kupata fursa hiyo watakaporudi katika maeneo yao.

Imeandikwa na Albano Midelo

Afisa Habari Manispaa ya Songea

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa