• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

VIPAUMBELE vitakavyoipaisha Manispaa ya Songea

Tarehe ya kuwekwa: May 14th, 2018

MANISPAA ya Songea iliyopo mkoani Ruvuma ni miongoni mwa Halmashauri nchini ambazo zimeweka dhamira ya kuhakikisha inaweka mikakati ya kuboresha maisha ili kuendana na kasi ya Rais wa awamu ya tano ya kujenga Tanzania mpya yenye neema.

Baraza la Madiwani la Manispaa hiyo likiongozwa na Mwenyekiti wake Mstahiki Meya Alhaj  Abdul Hassani Mshaweji kwa kushirikiana Mkurugenzi wa Manispaa hiyo Tina Sekambo pamoja na wataalam katika idara zote  wameweka maeneo kumi ya vipaumbele yatakayoiwezesha manispaa hiyo kupaa.

Halmashauri ya Manispaa  imeangalia maeneo ya msingi katika kuboresha  na kuimarisha utoaji wa huduma kwa kuyapa uzito maeneo hayo ili kukabiliana na  changamoto mbalimbali zinazojitokeza wakati wa utekelezaji wa majukumu ya msingi ya Halmashauri.

Vipaumbele ambavyo vimepitishwa na Baraza la madiwani la Halmashauri ya manispaa hiyo vimelenga katika Sekta ya Elimu ambapo Halmashauri imejiwekea malengo katika kuboresha huduma za jamii hasa katika kuboresha miundombinu ya shule za Msingi na Sekondari kwa kukamilisha miradi viporo na kujenga miundombinu mipya.

Baraza limeyataja Maeneo yatakayozingatiwa katika sekta ya elimu kuwa ni pamoja na ujenzi wa madarasa,maabara,mabweni,vyoo, ukarabati wa madarasa ununuzi wa samani pamoja na mishahara ya watumishi.

Sekta ya Afya  ni miongoni mwa vipaumbele vilivyopitishwa na Baraza hilo Lengo likiwa ni kuboresha miundombinu ya Vituo vya Afya na Zahanati kwa kuendeleza ujenzi na upatikanaji wa dawa. Maeneo muhimu ni ujenzi wa zahanati, ukarabati, ujenzi wa chumba cha upasuaji, samani na ununuzi wa madawa.

Kipaumbele kingine ambacho kimewekwa na Manispaa ya Songea kuwa ni Sekta ya Maji  Lengo likiwa ni kuongeza upatikanaji wa maji ya kutosha katika maeneo ya pembezoni ya Manispaa kwa kujenga visima vya maji  virefu na vifupi, kuanzisha uvunaji wa maji ya mvua na kuanzisha mtandao wa maji ya bomba.

Sekta ya ujenzi pia imepewa kipaumbele ambapo Manispaa ya Songea imejiwekea lengo la kuboresha miundombinu ya barabara kwa kufanya matengenezo ya mara kwa mara, maeneo korofi na matengenezo ya kawaida.

Kipaumbele pia kimewekwa katika Sekta ya Kilimo,Uvuvi Mifugo na Ushirika Lengo likiwa  ni kuendeleza kilimo bora na endelevu kwa kutumia pembejeo za kisasa kwa ajili ya kuongeza uzalishaji wa mazao ya chakula na biashara.

Sekta ya Mipango Miji, Ardhi na Maliasili  ni miongoni mwa vipaumbele vilivyopitishwa katika bajeti lengo likiwa ni kuboresha makazi ya wananchi kwa kuongeza upimaji wa viwanja, na ulipaji wa fidia kuboresha maeneo yaliyoendelezwa kiholela ambayo yamesababishwa na uhaba wa viwanja vilivyopimwa.

Masuala Mtambuka ambayo yamepewa kipaumbele katika manispaa ya Songea ni pamoja na kutoa elimu ya kujikinga na maambukizi ya maradhi mbalimbali kama UKIMWI, Malaria Kifua Kikuu na kushughulikia masuala ya UKIMWI, magonjwa ambayo hayapewi kipaumbele,Mazingira na kupambana na Madawa kulevya na rushwa.

Imetolewa na Albano Midelo

Afisa Habari Manispaa ya Songea

Mei 14,2018

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • Chupa 14,789 za Damu Kukusanywa Mkoani Ruvuma

    June 04, 2025
  • Mazishi ya Muasisi wa TANU Alhaji Mustapha Songambele

    June 03, 2025
  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • Tazama zote

Video

katibu Mkuu CCM Taifa Aongoza Maziko ya Alhaji Songambele
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa