• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

VIVUTIO vinavyofanana na vya Ujerumani vyagundulika Ifinga

Tarehe ya kuwekwa: July 24th, 2018

SEKTA ya Utalii katika mkoa wa Ruvuma inaendelea kufunguka baada ya kugundulika vivutio viwili vya utalii vilivyopo katika Halmashauri ya Madaba wilayani Songea mkoani Ruvuma.Vivutio hivyo ni bwawa ambalo linaitwa Beata lililopo kilometa nne toka katika Kijiji cha Ifinga .Kijiji cha Ifinga kipo umbali wa kilometa 48 toka barabara  kuu ya Songea -Njombe.Paroko wa Parokia ya Ifinga Padre John Otete ameongoza hadi kilipo kivutio hicho ambacho kiligundulika na wamisionari wa kijerumani miaka ya 1930.Bwawa hilo ambalo lipo kati kati ya milima lina urefu wa meta zaidi ya 500.Maajabu ya bwawa hilo ni kwamba muda wote maji yake ni masafi na kuna samaki wengi ambao wamekuwa kivutio.

Kulingana na padre Otete,wajerumani baada ya kugundua bwawa hilo na namna lilivyowavutia waliamua kulipa jina la Beata kwa kilatini likiwa na maana ya utukufu.Bwawa hilo lilikuwa linatumika na wamisionari hao kwa kufanya pikiniki na kuogelea na walipoondoka wenyeji wa eneo hilo walikuwa wanaliogopo kulitumia wakiamini ni bwawa la mizimu na masheni.Hata hivyo baada ya Padre huyo kupelekwa katika eneo hilo tangu mwaka jana ameamua kuwaelimisha wananchi wa Ifinga kuwa bwawa hilo ni kivutio cha utalii wanatakiwa kulilinda kwa kutoharibu mazingira yake ambapo hivi sasa wananchi wanafurahia kivutio hicho ikiwa ni pamoja na kunywa maji yake ambayo yanaradha ya aina yake.

Tayari wataalam wa misitu TFS wamekwenda katika eneo la bwwwa hilo na kupima eneo hilo ambalo lipo ndani ya eneo la parokia ya Ifinga.Licha ya kivutio hicho kivutio kingine ambacho kinavutia wengi wanaosafri toka Lilondo kwenda Ifinga ni milima ya kupendeza ambayo Padre Otete anaifananisha na milima ya nchi ya Ujerumani na kusisitiza kuwa milima hiyo kipindi cha masikina inavuti wengi ambao wamekuwa wanasimama na kufanya utalii wa picha.

"Mimi nikifikahapa najiona kama nipo Ujerumani,kwa sababu milima hii inafanana na sana na ile ambayo niliiona nchini Ujerumani",anasisitiza padre Otete.

Makala imeandikwa na Albano Midelo simu 0784765917

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa