• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

WAANDISHI WA HABARI MKOANI RUVUMA, " WAADHIMISHA SIKU YA UHURU WA VYOMBO VYA HABARI".

Tarehe ya kuwekwa: May 16th, 2022

Na,

AMINA PILLY,

AFISA HABARI MANISPAA.

16 MEI 2022

Waandishi wa habari Ruvuma watakiwa kutumia taaluma zao kuibua vitendo vya ukatili wa kijinsia kwa lengo la kuzuia na kutokomeza matukio hayo katika jamii.

Hayo yamebainishwa na Mwenyekiti wa maadili ya kamati  ya waandishi wa habari Mkoa wa Ruvuma Methew Ngalimanayo alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari pamoja na wadau wa habari kwenye maadhimisho ya siku ya  uhuru wa vyombo vya habari duniani ambapo kwa Mkoa wa Ruvuma yameadhimishwa  leo tarehe 16 Mei 2022 katika ukumbi wa Manispaa ya Songea.

Ngalimanayo pia ametoa rai kwa waandishi wa habari kuhakikisha usalama wao wakati wakitekeleza majukumu  yao na kufuata maadili ya uandishi wa habari pamoja na kutumia mbinu za kujilinda na matukio yenye kuathiri taaluma yake.

Ametoa wito kwa waandishi hao kutumia nafasi yao katika jamii kwa kuvitangaza vivutio mbalimbali vya utalii vilivyopo ndani ya Mkoa wa Ruvuma ili kuutambulisha Mkoa ndani na  nje ya nchi pamoja na kuvutia wawekezaji na kusaidia kukuza uchumi wa Mkoa na Taifa kwa ujumla.

Kwa upande wake Makamu Mwenyekiti wa Klabu ya waandishi wa habari Mkoa wa Ruvuma Amoni Mtega  alisema kuwa lengo la kuadhimisha siku hiyo ni kulinda hali ya uwepo wa uhuru wa vyombo vya habari na kujadili changamoto mbalimbali zinazowakabili waandhishi wa habari katika kutimiza majukumu yao pamoja na kutafuta ufumbuzi wa changamoto hizo.

Naye Katibu wa Klabu ya waandishi wa habari Mkoani Ruvuma Andrew Chatwanga alisema kuwa maadhimisho ya siku ya uhuru wa vyombo vya habari Tanzania yalianza kuadhimishwa rasmi mnamo mwaka 1993  baada ya kuratibiwa na  Umoja wa Mataifa kwa lengo la kutambua mchango wa sekta ya habari na kuangalia changamoto zinazoikumba sekta hiyo.

Akiwasilisha mada katika mkutano huo Mhdhili Dkt. Denis Mpagaze alisema kuwa miongoni mwa changamoto kubwa katika tasnia ya habari ni ukuaji wa teknolojia hali inayopelekea watu wasio waandishi wa habari kufanya kazi za habari kwa kutumia mitandao ya kijamii na kutoa taarifa ambazo siyo sahihi na zisizozingatia maadili ya uandishi wa habari.

Aliongeza kuwa ili kukabiliana na changamoto hizo Serikali iangalie namna ya kudhibiti hali hiyo kwa kuweka sheria kali zaidi pamoja na waandishi wa habari kwenda sambasamba na ukuaji wa teknolojia katika nyanja ya habari bila kuhatarisha maisha yao.

Naye Mkurugenzi wa Manispaa ya Songea Dkt. Frederick Sagamiko alisema kuwa Halmashautri ya Manispaa ya Songea itaendelea kushirikiana na waandishi wa habari Mkoani Ruvuma kwa lengo la kutoa taarifa ya utekelezaji wa shughuli mbalimbali za maendeleo kwa wananchi.

Dkt. Sagamiko ametoa rai kwa waandishi wa habari kushiriki katika kuleta maendeleo Mkoani Ruvuma kwa kutangaza fursa mbalimbali za maendeleo zinazopatikana ndani ya Mkoa kama vile uwekezaji wa viwanda na utalii.

Maadhimisho ya siku ya uhuru wa vyombo vya habari duniani hufanyika kila mwaka Mwezi Mei na kwa Mkoa wa Ruvuma yamefanyika leo na kuwashirikisha wanahabari na wadau mbalimbali wa habari wakiwemo viongozi wa Serikali ambapo maudhui ya maadhimisho hayo kwa mwaka 2022 yanasema “Uandishi wa habari na changamoto ya kidigitali”.

Mwisho.

 

 

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa