• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Wajasiliamali 200 wapata mafunzo ya usalama na afya mahali pa kazi

Tarehe ya kuwekwa: April 24th, 2017

WAJASIRIMALI wadogo 200 wa Manispaa ya Songea wamepata mafunzo ya siku mbili ya usalama na afya mahali pa kazi  ambayo yametolewa na Wakala wa Usalama na Afya Mahali pa Kazi(OSHA).

Mkurugenzi wa Mafunzo,Utafiti na Takwimu wa OSHA Joshua Matiko akizungumza kwenye mafunzo hayo ambayo yamefanyika kwenye ukumbi wa Songea Club,alisema OSHA imekuwa na desturi ya kutumia mwezi Aprili kila mwaka kuelezea kazi mbalimbali zinazolenga kuboresha hali ya usalama na afya mahali pa kazi.

Alisema kila mwaka Aprili 28 ni siku ya maadhimisho ya siku ya usalama na afya mahali pa kazi duniani ambapo OSHA hutumia maadhimisho hayo kuhamasisha usajiri wa maeneo ya kazi,vikao vya wadau na makongamano ya watalaam wa masuala ya afya na usalama.

“Tunatumia maadhimisho hayo pia kwa kutoa vipindi vya elimu katika vyombo vya habari,maonesho ya usalama na afya na mafunzo ya usalama na afya kwa wajasirimali wadogo kama inavyofanyika hapa Songea’’,alisema Matiko.

Hata hivyo alisema mafunzo hayo ambayo yanatolewa bure yamelenga kuziba mwanya wa elimu ya usalama na afya kazini uliopo baina ya Taasisi na kampuni katika sekta rasmi na wazalishaji wadogo ambao hawajaweza kufikiwa katika mfumo rasmi wa serikali wa kusimamia afya na usalama wa wafanyakazi.

Akizungumza katika ufunguzi wa mafunzo hayo,mgeni rasmi Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Dk.Binilith Mahenge amewapongeza wakala wa serikali OSHA kwa kuanzisha mpango wa mafunzo hayo ambapo amewaomba waangalie uwezekano wa kuyaboresha zaidi mafunzo hayo ili yawafikie watanzania wengi.

Kwa upande wake Meneja wa OSHA Kanda ya Kusini Wilbert Ngowi alisema Mafunzo hayo ni mwendelezo wa mafunzo ya afya na usalama mahali pa kazi ambayo yalifanyika mwaka jana katika nchi nzima  yakishirikisha jumla ya wajasiriamali wadogo 1830 ambapo mwaka huu mafunzo hayo yameshirikisha wajasirimali wadogo 2500.

Kulingana na Ngowi,wajasirimali hao wamejifunza mada mbalimbali zikiwemo majukumu ya msingi yanayofanywa na OSHA,maana ya usalama na afya mahali pa kazi,namna ya kuvitambua vihatarishi vilivyopo sehemu za kazi,kujikinga na ajali na elimu ya huduma ya kwanza.

Taarifa imetolewa na 

Albano Midelo

Afisa Habari na Mawasiliano Manispaa ya Songea

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa