• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

WAJASIRIAMALI 380 wapata mafunzo ya uwekezaji

Tarehe ya kuwekwa: April 20th, 2018

WAJASIRIMALI wadogo wapatao 380 kutoka vikundi 67 katika Halmashauri ya Manispaa ya Songea mkoani Ruvuma wamepata mafunzo ya mbinu za uwekezaji katika viwanda vidogo.

Mafunzo hayo ambayo yamefanyika kwenye ukumbi wa Songea Klabu mjini Songea, yameratibiwa na Idara ya Maendeleo ya Jamii Manispaa ya Songea,na kufundishwa na watalaam mbalimbali wa Taasisi na asasi za kifedha za serikali.

Akisoma taarifa ya vikundi hivyo,Mkuu wa Idara ya Maendeleo ya Jamii katika Manispaa hiyo,Naftari Saioloyi amesema Manispaa ya Songea imekuwa na utaratibu wa kukopesha vikundi vya wanawake na vijana kutoka katika mapato yake ya ndani.

Amesema katika kipindi cha mwaka wa fedha wa 2017/2018,jumla ya vikundi 102 vilikopeshwa shilingi milioni 116 kati ya hizo vikundi 87 vya wanawake vilikopeshwa Zaidi ya milioni 101 na vikundi vya vijana 15 vilikopeshwa  shilingi milioni 14.9.

“Mikopo hii ililenga katika kila kikundi kuendeleza miradi ambayo ilianzishwa.Leo hii Manispaa ya Songea imeona ni vyema viongozi wa wanavikundi kukutana na wataalam toka Taasisi za serikali za SIDO,VETA na wataalam wa Benki ili wapate mafunzo na kuweza kupanua wigo wao wa uwekezaji’’anasisitiza Saioloyi.

Ameongeza kuwa mafunzo hayo yataviwezesha vikundi kutafakari kulingana na maeneo wanayotoka,rasimali walizonazo na upatikanaji wa soko kwa mazao watakayozalisha.

Akizungumza kabla ya kufungua mafunzo hayo,mgeni rasmi Mkuu wa wilaya ya Songea Pololet Mgema amesisitiza kuwa mafunzo hayo ni muhimu hasa katika kutekeleza kauli mbiu ya serikali inayolenga Tanzania ya viwanda na kwa kila mkoa kuwa na viwanda 100.

Amesema kuwa wajasirimali wadogo watakapofanikisha kwenye uwekezaji hata kama ni wa kiwanda kidogo sana,watakuwa kwenye malengo ya Taifa ya viwanda.

“Hakuna aliyezaliwa akaanza kutembea,bali huanzia kutambaa,kusimama halafu kutembea,kiwanda kidogo kinaanza na mtaji mdogo,anzeni sasa na mtayaona mabadiliko’’, anasisitiza Mgema.

Mafunzo ya mbinu za uwekezaji katika viwanda mdogo yametolewa na Taasisi za serikali  nchini ambazo ni SIDO,VETA,TCCIA na Benki za NMB,CRDB na POSTA.

Imetolewa na Albano Midelo

Afisa Habari Manispaa ya Songea

Aprili 20,2018

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa