• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

WALIMU Manispaa ya Songea waaswa kuvuta subira

Tarehe ya kuwekwa: June 28th, 2018

WALIMU katika Halmashauri ya Manispaa ya Songea mkoani Ruvuma ambao walipata barua za kupandishwa madaraja na bado hawajarekebishwa mishahara yao wameomba kuvuta subira kwa kuwa serikali kila mwezi inarekebisha mishahara ya walimu waliopandishwa vyeo.

Afisa Utumishi Mkuu wa Manispaa hiyo Lewis Mnyambwa amesema majina ya walimu wote ambao walipandishwa madaraja yao katika mwaka wa fedha wa 2015/2016 yameingizwa kwenye mfumo wa taarifa za kiutumishi na mishahara na kwamba kila mwezi kuna baadhi ya walimu ambao wanarekebishiwa mishahara yao.

Amesema katika Halmashauri ya Manispaa ya Songea idadi ya walimu waliopata barua za kupandishwa madaraja ni 704 na kwamba idadi hiyo ni kubwa hivyo walimu wanatakiwa kuwa na subira kwa kuwa serikali imekuwa inarekebisha mishahara yao kila mwezi.

"Sisi kama Idara ya Utumishi Manispaa ya Songea, tumeshakamilisha kazi ya kuyaingiza majina yote kwenye mfumo wa serikali wa utumishi na mishahara,majina ya walimu hao yapo pending kila mwezi kuna walimu wanarekebishiwa mishahara yao,naomba wawe wavumilivu'',anasisitiza Mnyambwa.

Hata hivyo amesema hadi sasa walimu zaidi ya 100 tayari wamerekebishiwa mishahara yao na kwamba suala la kurekebisha mishahara ya walimu waliopandishwa vyeo sasa lipo katika ngazi ya kitaifa hivyo walimu wanatakiwa kuwa wavumilivu.

Akizungumza siku ya sikukuu ya wafanyakazi Mei Mosi mwaka huu iliyofanyika mjini Iringa,Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.John Magufuli alisema serikali nchini imewapandisha vyeo wafanyakazi Zaidi ya 88,000 na kwamba  wafanyakazi zaidi ya 25,000 wanatarajiwa kupandishwa madaraja yao mwaka mpya wa fedha 2018/2019.

Rais Magufuli aliwahakikishia watumishi kuwa serikali itaendelea kuwapandisha vyeo wafanyakazi kadri bajeti itakavyoruhusu na kwamba   watumishi wote wanaodai madeni halali watalipwa fedha zao.

Imetolewa na Albano Midelo

Afisa Habari Manispaa ya Songea

Juni 28,2018.

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa