• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Wananchi Songea kusahau shida ya Maji

Tarehe ya kuwekwa: April 6th, 2017

Wananchi Songea kusahau shida ya maji

MRADI wa maji uliofadhiliwa na Benki ya Dunia katika Mtaa wa Ruhuwiko Kanisani Manispaa ya Songea uliogharimu sh.milioni 488.67 unatarajiwa kukabidhiwa kwa wananchi hivi karibuni. Utekelezaji wa mradi huo ulioanza mwaka wa fedha wa 2013/ 2014 umefikia asilimia 95.Mradi huo unaojengwa na Mkandarasi Giraf Investment Co.Ltd ulitarajiwa kukamilika katika mwaka wa fedha wa 2014/2015. Hata hivyo mradi huo ulisimama kutokana na ukosefu wa fedha za kumlipa Mkandarasi kutoka serikali kuu.Mkandarasi wa mradi huo hadi sasa amelipwa sh.milioni 358.36 ambapo katika mwaka wa fedha wa 2016/2017,serikali imeleta fedha kiasi cha zaidi ya sh.milioni 62 kwa ajili ya kukamilisha mradi huo. 

Kwa upande wake Mhandisi wa Maji katika Manispaa ya Songea Samwel Sanya amezitaja kazi ambazo zimefanyika hadi sasa katika mradi huo kuwa ni ujenzi wa nyumba mbili za mitambo,ujenzi wa bomba kuu la la mm 0.75,bomba la kusambaza maji la mm 9.8,ufungaji wa pampu mbili,ujenzi wa tanki la lita 135,000 na ujenzi wa vituo 11 vya kuchotea maji. “Kazi zilizobakia na Mkandarasi anaendelea kukamilisha ni kujenga chemba za pampu na valvu,kujenga vituo vinne vya kuchotea maji,ujenzi wa uvunaji maji ya mvua na kufanya marekebisho yote yaliyojitokeza wakati wa ujenzi’’,amesema Sanya. 

Sanya amezitaja changamoto za mradi huo kuwa ni Manispaa kutopata fedha za kukamilisha mradi toka serikali kuu kwa wakati na wananchi kuwa na uelewa mdogo wa uchangiaji na uendeshaji wa miradi ya maji. Watu wapatao 3,447 kutoka katika Mtaa wa Ruhuwiko wanatarajia kunufaika na mradi huo wa maji safi na salama baada ya mradi kukamilika hivi karibuni na kukabidhiwa wananchi kabla ya mwezi Juni mwaka huu.

Taarifa imetolewa na Albano Midelo
Afisa Habari na Mawasiliano wa Manispaa ya Songea



Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • Bil. 22.9 Kujenga Masoko ya Kisasa Manzese A na B, na Kiwanda cha Kuchakata Mazao ya Nafaka Lilambo

    July 06, 2025
  • MBUNGE SONGEA MJINI AKABIDHI KOMPYUTA NA KUFADHILI UKARABATI WA OFISI ZA POLISI

    June 27, 2025
  • DC Songea bAzindua Dawati la Huduma za Ustawi wa Jamii Stendi ya Mabasi Songea

    June 24, 2025
  • Meya Mbano; Amewataka Wananchi Kulinda Haki za Watoto

    June 16, 2025
  • Tazama zote

Video

Makabidhiano ya Mkataba Soko la Manzese A&B
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa