• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

WANANCHI washauriwa kutembelea Makumbusho ya Taifa ya Majimaji

Tarehe ya kuwekwa: August 24th, 2019

Uongozi wa Makumbusho ya Majimaji umewataka wanajamii kutambua umuhimu wa kutembelea Makumbusho ya Mashujaa wa vita vya Majimaji Songea Mkoani Ruvuma.

Mhifadhi kiongozi Adson  Ndyanabo ameeleza hayo ofisini kwake katika mahojiano maalumu kuwa Makumbusho hayo yana manufaa kwa jamii na taifa kwa ujumla kwa kuwa yanaongeza  mapato na kutoa ajira rasmi na zisizo rasmi kwa wananchi.

Amesema Makumbusho hayo pia yanahifadhi historia,,hutoa elimu kwa jamii ili kutambua tulipotoka, tulipo pia ni utambulisho wa jamii husika .

Ndyanabo amevitaja vivutio mbalimbali vya utalii vinavyopatikana katika Makumbusho ya Majimaji kuwa  ni  Chandamali ambapo kuna mapango yaliyokuwa makazi ya Nduna Songea Mbano, Mahenge ambapo kuna majengo ya Makumbusho, makaburi, sanamu za Mashujaa na vifaa walivyokuwa wakitumia katika maisha yao vikiwemo vya asili na kiutamaduni na Songea Club ambapo Wajerumani walitumia eneo hilo  kunyongea Mashujaa.

Amezitaja changamoto mbalimbali zinazowakabili ikiwemo wito mdogo kwa wanajamii kwani watalii  wanaotembelea Makumbusho hayo wengi wao  ni wageni , hali ngumu ya maisha imesababisha kupungua kwa idadi ya watalii pia mtazamo wa watu wa elimu bure umeathiri utalii kwasababu imekuwa ngumu kwa wazazi kutoa michango inayowezesha wanafunzi kutembelea vivutio vya utalii  kwani wanafunzi walikuwa watalii wakubwa katika vivutio hivyo.

“Kama mtu anashindwa kumtembelea ndugu yake hawezi kutembelea Makumbusho, pia watanzania wengi hawana utamaduni wa kutoka” Amesema Ndyanabo.

Makumbusho ya Majimaji  kwa mwaka 2018 na 2019 imetembelewa na wageni wasiozidi   1500  ambayo amesema  ni ndogo.Ametoa rai kwa serikali  kutangaza vivutio vya utalii kwenye vyombo mbalimbali vya habari  ndani na nje ya nchi ili  kuongeza idadi ya watalii.

Makumbusho ya Taifa ya Majimaji ni miongoni mwa Makumbusho saba za taifa zilizopo Nchini Tanzania ambayo ilijengwa mwaka 1980.

Imeandaliwa na 

Elika Mwakinandi

Wa kitengo cha TEHAMA Manispaa ya Songea

23 August, 2019.

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MBUNGE SONGEA MJINI AKABIDHI KOMPYUTA NA KUFADHILI UKARABATI WA OFISI ZA POLISI

    June 27, 2025
  • DC Songea bAzindua Dawati la Huduma za Ustawi wa Jamii Stendi ya Mabasi Songea

    June 24, 2025
  • Meya Mbano; Amewataka Wananchi Kulinda Haki za Watoto

    June 16, 2025
  • Meya wa Songea Atoa Wito kwa Familia Kuchangia Damu Kuokoa Maisha.

    June 14, 2025
  • Tazama zote

Video

Mbunge Akabidhi Kompyuta 6 na Kufadhili Ukarabati wa Ofisi za Polisi
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa