• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

WAPIGWA faini ya milioni moja kwa kukataa kuchangia usafi

Tarehe ya kuwekwa: March 26th, 2018

WATU kumi toka katika Kata za Majengo, Misufini, Bombambili,Matarawe na kata ya mjini Manispaa ya Songea wamepigwa faini ya jumla ya shilingi milioni moja na Mahakama ya Mwanzo ya Mfaranyaki baada ya kukataa kulipa shilingi 2000 inayotozwa kila mwezi kwa kila kaya kuchangia usafi wa mazingira.

Mkuu wa Idara ya Usafi na Mazingira Manispaa ya Songea Philipo Beno amesema wameamua kuanza kuchukua hatua ya kuwapeleka mahakamani wananchi wote wanaokaidi kulipa mchango huo hali ambayo inawakatisha tamaa wananchi ambao wanachangia.

‘‘Sheria imepitishwa na wananchi wa Manispaa ya Songea kila mwezi kuchangia shilingi 2000 kwa kila kaya na kwa wafanyabiashara shilingi 4000 ambayo imepitishwa kuchangia usafi wa mazingira katika mitaa na kata za Manispaa’’,anasisitiza Beno.

Amesema wananchi hao kwa nyakati tofauti baada ya kukataa kuchangia kiasi hicho cha fedha walipelekwa mahakamani ambako wamepigwa faini ya shilingi 100,000 kila mmoja kati ya fedha hizo Manispaa inachukua shilingi 50,000 na mahakama shilingi 50,000 na kwamba kuanzia sasa zoezi la kupeleka mahakamani wanaogoma kuchangia usafi wa mazingira litakuwa endelevu.

Katika hatua nyingine Mkuu wa Wilaya ya Songea Pololet Kamando Mgema amemwagiza Mkurugenzi wa Manispaa ya Songea kupitia kwa maafisa afya kuwapiga faini ya shilingi 50,000 kwa kila mwananchi ambaye hatashiriki usafi  Jumamosi ya kila mwisho wa mwezi ambayo ni siku maalum ya kufanya usafi katika maeneo ya umma.

Mgema amekuwa anatoa agizo hilo kila Jumamosi ya mwisho wa mwezi kutokana na baadhi ya wananchi kutoshiriki kufanya usafi siku hiyo ambayo imeagizwa kisheria wananchi wote kushiriki.


Sheria ya usafi wa mazingira inawatia hatiani wale wote waliosababisha kuwepo kwa uchafu na wale wanaokataa kufanya usafi wa Mazingira na kwamba adhabu yake ni faini ya sh 50,000 .

Mkuu wa wilaya amewaagiza watendaji wa mitaa kuwaandika majina wananchi wanaoshiriki usafi wa Mazingira kila Jumamosi ya mwisho wa mwezi na kwamba wale wote ambao hawafiki wapigwe faini kulingana na sheria iliyopo.

Mkuu pia amezikumbusha kaya zote katika mitaa 95 ya Manispaa ya Songea kuchangia mchango wa usafi wa Mazingira sh.2000(Elfu mbili) na wafanyabiashara shilingi 4000 ambao unafanyika kila mwezi.

Usafi wa Mazingira ni jambo la lazima ili kukabiliana na magonjwa yanayosababishwa na uchafu kama vile kipindupindu na malaria.

 Utafiti umebaini kuwa katika nchi zilizoendelea hakuna watu wanaougua magonjwa yanayotokana na uchafu na kwamba nchi hizo zinashangaa kuona kuna watu wanaugua na kufa kutokana na magonjwa yanayosababishwa na uchafu.

Imetolewa na Albano Midelo

Afisa Habari Manispaa ya Songea

Machi 26,2018

 

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa