Na, Amina Pilly.
Makamu Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Bara, Stephen Wasira, ameendelea na ziara yake mkoani Ruvuma, akihitimisha ziara hiyo leo, Juni 12, 2025, katika Manispaa ya Songea. Katika ziara hiyo, Wasira amewataka Watanzania kulinda amani na kudumisha mshikamano, akisisitiza kuwa uvunjifu wa amani, udini, na ukabila hautakiwi katika jamii.
Aidha, Wasira amewasihi viongozi wa CCM na wananchi kwa ujumla kuwa na umoja na ushirikiano ili kuhakikisha maendeleo endelevu yanapatikana katika maeneo yao. Amesisitiza kuwa CCM itaendelea kushika dola kwa sababu ya sera zake bora zinazolenga kuboresha maisha ya wananchi, huku akisisitiza kuwa vyama vya upinzani haviwezi kushindana na CCM kwa sababu ya migogoro ya ndani na ukosefu wa mshikamano miongoni mwao.
Ziara hii ya Wasira ni sehemu ya juhudi za chama hicho kuhakikisha utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM na kuimarisha uhai wa chama katika maeneo mbalimbali nchini ambayo imehitimishwa leo tarehe 12 juni 2025 katika uwanja wa Shule ya Msingi Matarawe Manispaa ya Songea.
SONGEA MUNICIPAL COUNCIL
Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA
Simu ya Mezani: 025 2602970
Simu ya Kiganjani:
Barua Pepe: info@songeamc.go.tz
Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa