• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

WATUMISHI MKOANI RUVUMA WAPEWA MAFUNZO YA MFUMO WA TATHIMINI YA MAHITAJI YA RASILIMALI WATU

Tarehe ya kuwekwa: November 21st, 2023

Katika kufanikisha usimamizi wa utendaji kazi katika utumishi wa umma kila mtumishi wa umma alikuwa anapimwa utendaji wake wa kazi kwa kutumia mfumo wa siri uliojulikana kama ‘‘Taarifa ya Siri ya Utendaji Kazi ya Mtumishi wa Serikali’’(Confidential Appraisal System).

Ambapo  Kuanzia mwaka 2004 hadi mwaka 2023, utendaji kazi wa Watumishi wa Umma umekuwa ukipimwa kwa kutumia Mfumo wa Wazi wa Mapitio na Tathmini ya Utendaji Kazi (Open Performance Review and Appraisal System - OPRAS), pia kuanzia Mwaka 2018 hadi 2023, kwa upande wa taasisi, ilikuwa na Mfumo wa mikataba ya Utendaji Kazi katika Taasisi za Umma (Institutional Performance Contracting System (IPCS).

Aidha, 2023 na kuendelea, utendaji kazi wa mtumishi wa umma na utendaji kazi wa taasisi ya umma utasimamiwa na Mfumo wa Usimamizi wa Utendaji Kazi  katika Utumishi wa Umma ambao una sehemu mbili ambazo ni Public Employees Performance Management Information System (PEPMIS) ambao ni sehemu ya kwanza ya Mfumo Mpya wa Usimamizi wa Utendaji Kazi ambao unachukua nafasi ya OPRAS,  na Public Institutions Performance Management Information System (PIPMIS) ni sehemu ya pili ya Mfumo Mpya wa Usimamizi wa Utendaji Kazi  ambao unachukua nafasi ya IPCS katika kupima utendaji kazi wa Taasisi ya Umma.

Hayo yamejiri wakati wa mafunzo ya Mfumo wa thamani ya mahitaji ya Rasilimali watu Mkoani Ruvuma inayofanyika katika ukumbi wa Manispaa ya Songea kuanzia 20Novemba hadi 24 Novemba 2023 ambayo yamehudhuriwa na wakuu wa Idara na Vitengo kutoka  Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma, Halmashauri ya Wilaya ya Songea, pamoja na Halmashauri ya Manispaa ya Songea kwa lengo la Kuwezesha Mamlaka za Serikali za Mitaa na taasisi nyingine katika Mkoa kufanya Tathmini ya Rasilimali watu katika Mkoa na kubaini Mahitaji ya Rasilimali watu.

Akizungumza Mkurugenzi Maendeleo ya Sera Ofisi ya Rais Menejiment na Utumishi wa Umma na Utawala Bora Bw. Cyrus Kapinga alisema “Mfumo wa Tathmini ya Mahitaji ya Rasilimaliwatu uliokuwa unatumika kwa muda mrefu katika Taasisi za Umma ulikuwa ni  wa kutumia Job List Forms  ambapo ulikuwa unatumia vigezo mbalimbali katika kubaini mahitaji ya watumishi ikiwemo, Muundo na Mgawanyo wa Mahitaji,  Sheria na Miongozo mbalimbali iliyopo, na  kazi zinazofanyika kwa mzunguko yaani  shift.”

 Mfumo huo wa kuandaa mahitaji kwa kutumia Joblist Forms  umekuwa na changamoto kutokana na kutumia zaidi njia ya majadiliano na hivyo kusababisha maamuzi ya idadi ya watumishi wanaohitajika kutegemea zaidi utashi wa mwenye Taasisi na Mwezeshaji, ambapo licha ya kutumika kwa Mfumo huo bado kumekuwepo na changamoto mbalimbali ambazo ni pamoja na Malalamiko ya waajiri kuhusu upungufu/uhaba wa watumishi, Kukosekana  kwa takwimu sahihi zinazoongoza Waajiri katika kuandaa maombi ya ajira mpya, Kukosekana takwimu sahihi zinazoongoza OR MUUUB kutoa vibali vya ajira,  na takwimu za mahitaji ya watumishi yanayoandaliwa na Waajiri kuwekwa katika Mfumo wa taarifa za Watumishi na Mishahara (HCMIS) kutokuwa halisia.

Hata hivyo, Ili kuondokana na changamoto hizo Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora ilichukua hatua ya ujenzi wa Mfumo wa Tathmini ya Rasilimaliwatu (HR Assessment System) ambao ni Mfumo wa kisayansi  unakokotoa mahitaji ya watumishi kwa kufanya  uchambuzi  wa uzito wa majukumu (Work Load Analysis),  pia unawewezesha kubaini mahitaji ya Kada ya Walimu nchi nzima kwa kutumia njia ya uwiano  na  Mahitaji ya Maafisa, Maafisa wasaidizi, pamoja na Viongozi na kada saidizi kwa kutumia fomu maalum katika mfumo. Bw. Kapinga “alibainisha”.

 

Amewataka watumishi wote  kutenga muda kwa ajili ya kufanikisha zoezi hilo na kutoa ushirikiano wa pamoja na kuwa tayari kupata mafunzo ya Mfumo wa Usimamizi wa Utendaji Kazi katika Utumishi wa Umma (PEPMIS/PIPMIS) na Mfumo wa HR Assessment pamoja na  kutekeleza majukumu watakayopewa na wataalam wa  Mifumo  ya PEPMIS/PIPMIS na HR Assessment.

 

 IMEANDALIWA NA;

AMINA  PILLY;                                                                   

KITENGO CHA MAWASILIANO SERIKALINI.





Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa