• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

WATUMISHI wa Wizara ya Kilimo nchini watakiwa kuongeza Tija katika uzalishaji wa mazao

Tarehe ya kuwekwa: September 16th, 2019

Waziri wa Kilimo Japeth Hasunga amewaagiza watumishi wa wizara yake kufanya kazi kwa uadilifu na uzalendo ili kuongeza uzalishaji wa mazao nchini.

Amewataka wataalamu kuzingatia dira ya wizara ili kukifanya kilimo kuwa cha kibiashara na cha faida kwa wakulima kote nchini.

Waziri Hasunga ametoa agizo hilo Ijumaa (13.09.2019) wakati alipofanya kikao cha kazi na wafanyakazi wote wa wizara ya kilimo waliopo makao makuu Jijini Dodoma.

“Lengo la wizara yetu ni kuhakikisha nchi inazalisha mazao ya kutosha na kuwa na utoshelevu na usalama wa chakula muda wote” alisema Waziri

Alieleza katika kikao hicho kuwa uzalishaji wa mazao ya  chakula umewezesha nchi kuwa na utoshelevu asilimia 124 mwaka 2018  na asilimia 119 mwaka 2019

Waziri Hasunga aliwataka watumishi wa wizara hiyo kuweka mipango inayotekelezeka kitaalam ili kujibu hitaji la wakulima nchini ikiwa ni pamoja na elimu ya kilimo cha kisasa na chenye tija katika eneo dogo.

“Andikeni miradi ili wizara ipate pesa zaidi za kutekeleza shughuli za uzalishaji mazao nchini na badala ya kutegemea bajeti ya serikali ili kufikia tija ya uzalishaji” Waziri Hasunga

Alisema Tanzania ina hekta milioni 44 zinazofaa kwa kilimo cha mazao mbalimbali lakini hali ya uzalishaji imeendelea kushuka kila mwaka kutokana na wataalam kutotimiza majukumu yao.

Ili kufikia uzalishaji mkubwa na wenye tija amewashauri wataalam wa wizara ya kilimo kujifunza uzoefu na teknolojia iliofikiwa na nchi za Kenya,Rwanda na Israel ambazo zimepiga hatua kubwa kuzalisha mazao katika eneo dogo.

“Israel, Rwanda na Kenya wanafanya vizuri katika uzalishaji,kajifunzeni ili tubadilishe kilimo chetu kiwe na mchango mkubwa zaidi kwenye pato la taifa ” alisisitiza Waziri

Kwa upande wake Naibu Waziri wa Kilimo Omary Mgumba akizungumza kwenye kikao hicho aliwasihi wafanyakazi kujituma na kutumia vizuri fedha za umma  ili miradi inayotekelezwa na wizara iwanufaishe wakulima.

Mgumba aliwataka watumishi hao kuongeza weledi wa ufanyaji kazi ili kupunguza gharama za uzalishaji na mkulima apate bei nzuri ya mazao yake sokoni.

Naye Naibu Waziri wa Kilimo Hussein Bashe alisisitiza suala la matumizi ya Tehama kuzingatiwa katika kuongeza ufanisi wa kazi za wizara ikiwa ni pamoja na upatikanaji wa takwimu sahihi za mazao na utendaji kazi.

Bashe aliwakumbusha watumishi hao kuwa wizara ya kilimo ndio imeajili watu asilimia 70 hivyo mafanikio ya utekelezaji wa Ilani yakiendelezwa yatasaidia Chama cha Mapinduzi kuendelea kuungwa mkono na wananchi.

“Uwepo wa Chama cha Mapinduzi madarakani utaimarika zaidi endapo sekta hii ya kilimo iliyoajili watanzania wengi itatoa mchango unaokusudiwa katika uchumi”alisema Naibu Waziri Bashe.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo Mhandisi Matherw Mtigumwe alimshukuru na kumhakikishia Waziri Hasunga kuwa wataalam walio chini yake wataongeza kasi katika ufanyaji kazi ili wizara ifikie malengo ya nchi .

Wizara ya kilimo ina watumishi 974 kati yao watumishi 452 wapo makao makuu na wengine 522 wapo kwenye taasisi, vyuo na wakala nchini.

Imeandaliwa na:

Kitengo wa Mawasiliano Serikalini

Wizara ya Kilimo-DODOMA

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa