• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

WAUMINI wachangia zaidi ya milioni 113 ujenzi wa Kanisa

Tarehe ya kuwekwa: October 18th, 2018

WAUMINI wa kanisa la Anglikana Mtaa wa Mtakatifu Augustino Mjimwema Dayosisi ya Ruvuma wamechangia zaidi ya shilingi milioni 113 kwa ajili ya ujenzi wa kanisa lao.

Akitoa taarifa ya ujenzi wa kanisa hilo kwa Askofu wa Dayosisi ya Ruvuma Mhashamu Raphael Haule,Katibu wa Kanisa hilo Dk.Daniel Mtamakaya amebainisha kuwa kati ya fedha hizo shilingi zaidi ya milioni 111 zimetumika ambapo katika kipindi cha Januari hadi Oktoba mwaka huu zaidi ya milioni 66 zimetumika.

Dk.Mtamakaya amebainisha matumizi ya fedha hizo kuwa zaidi ya milioni 47 zimetumika kwa ajili ya ujenzi wa boma,zaidi ya milioni 10 kwa ajili ya ununuzi wa bati katika awamu ya kwanza na boriti zimetumika zaidi ya milioni 12.

Matumizi mengine kulingana na Katibu huyo wa Kanisa,ni shilingi milioni nne gharama za fundi wa kuezeka,madirisha zaidi ya milioni 10 na kwamba kiasi kingine cha fedha kimetumika kwa ajili ufundi gibro,miundimbinu ya kanisa,umeme,mchanga,nyumba ya padre,kokoto,saruji na nondo.

“Kanisa limefanikiwa kununua ardhi yenye ukubwa wa hekari 100,kanisa limefanikiwa kusimamia kwaya yetu ya Mtakatifu Augustino kurekodi video,tunatarajia uzinduzi wa kwaya hiyo kufanyika hivi karibu,pia kanisa linaendesha semina za ndani kwa viongozi wa kanisa’’,amesisitiza Dk.Mtamakaya.

Kwa upande wake Padre wa Mtaa wa Kanisa hilo Padre John Midelo ameyataja matarajio ya kanisa hilo kuwa ni kuanza maandalizi ya ujenzi wa zahanati na uanddaaji wa mashamba mara baada ya ukamilishaji wa Hati.

Amesema kanisa linafanya ushirikishaji mkubwa kwa waumini katika kuendeleza kanisa na kwamba mkazo umewekwa kila waumini wanaoishi bila ndoa,wanashauriwa kufunga ndoa.

“kanisa hili linategemea zaidi rasilimali watu(waumini) katika kupata mapato yake ambapo mahudhurio katika ibada yamekuwa ni wastani wa waumini 106 ambao wanatoa wastani wa zaidi ya shilingi 80,000 kila siku ya bwana’’,anasisitiza Padre John.

Akizungumza katika Ibada ya utoaji wa Sakramenti ya Kipaimara kwa watoto 26 katika kanisa hilo,Askofu Haule amewapongeza waumini hao kujenga kanisa kubwa na linalovutia na kwamba hilo limewezekana kutokana na kusimama katika imani.

“Kilichowasimamisha hadi kujenga kanisa hili ni imani,kwa hiyo kwa imani tunaweza kufanya mambo makubwa ambayo,ndiyo maana Mungu amemleta roho Mtakatifu ili kukuza imani yetu’’,amesisitiza Askofu Haule.

Imeandaliwa na Albano Midelo,mawasiliano 0784765917

 

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa