• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

WAZEE WAJITOKEZA KWA WINGI KUPIMA AFYA ZAO, KUELEKEA SIKU YA WAZEE DUNIANI.

Tarehe ya kuwekwa: October 2nd, 2020

Tanzania huungana na nchi nyingine  wanachama wa Umoja wa Mataifa  katika kuadhimisha siku ya wazee Duniani, kwa ustawi wa wazee ambayo hauadhimishwa kila ifikapo tarehe 01 oktoba ya kila mwaka ambapo siku hii ilitengwa na baraza la Umoja wa mataifa kupitia azimio namba 45/106 la mwaka 1990.

 Kauli hiyo imetolewa jana  katika maadhimisho ya siku ya Wazee Duniani iliyofanyika katika uwanja wa Majimaji Manispaa ya Songea wenye lengo  kuu la  Kuelimisha na Kujenga hamasa na uelewa katika kuboresha upatikanaji wa huduma na haki za wazee katika Jamii.

Mgeni rasmi katika maadhimisho hayo alikuwa Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Christina Mndeme ambaye aliwakilishwa na Afisa Ustawi wa jamii Mkoa wa Ruvuma Victor Nyenza ambapo alianza  kwa kutembelea vibanda vya maonesho mbalimbali pamoja na vibanda vya upimaji wa afya.

Nyenza aliwapongeza wazee hao kwa kushiriki maadhimisho siku ya wazee duniani kwa kupima afya zao ambapo wazee waliojitokeza kupima uzito na  sukari walikuwa  37 kati ya hao (me 25, na  ke 12), waliopima vvu ni  67 kati ya hao (me 38 ) na (ke 29).

Awali katika taarifa  iliyosomwa na  Wazee wa baraza hilo ambayo ilisema nanukuu  “tunakuomba utufikishie shukrani zetu za dhati kwa Mheshimiwa Rais wetu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dr. John Joseph Pombe Magufuli kwa kuifikisha nchi yetu hapa tulipo katika awamu yake ya kwanza ya miaka mitano kwa kushugulikia masuala yanayowahusu wazee pamoja kuwawezesha watoto wetu toka ngazi ya shule za awali hadi sekondari kupata elimu bure, pamoja na Kuwepo kwa wizara maalumu inayosghulikia masuala ya wazee. “ mwisho wa kunukuu.

Wakizitaja baadhi ya changamoto zinazowakabili wazee hao ni kukosa fursa ya kupata mikopo kama inavyotolewa kwa vijana, wanawake na wenye  ulemavu, pamoja na  kutokuwepo kwa baraza huru la wazee ngazi ya mkoa,

Nyenza  akitolea majibu  kwa baadhi ya changamoto zilizotajwa na wazee hao ambapo aliahidi kuzichukua na kuzipeleka ofisi husika kwa ajili ya kuzishughulikia mapema iwezekanavyo.

Alibainisha kuwa kila mmoja wetu anawajibu wa kuwatunza wazee ili waweze kuwa azina ya baadaye na kujenga  kizazi chenye uzalendo  ambacho kitarithi desturi ya kuwapenda na kuwatunza wazee.

Kauli mbiu ya mwaka huu 2020 “Familia na Jamii tuwajibike kuwatunza wazee’’

IMETAYARISHWA NA;

AMINA PILLY;

AFISA HABARI MANISPAA YA SONGEA.

02 octoba 2020

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa