• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

WAZEE, WALEMAVU, AKINAMAMA WAJAWAZITO, NA WAGONJWA KUPEWA KIPAUMBELE SIKU YA UPIGAJI KURA .

Tarehe ya kuwekwa: October 25th, 2020

Tume ya Taifa ya uchaguzi (NEC) inaendelea kutoa mafunzo kwa wasimamizi wasaidizi wa vituo vya kupigia kura yanayoendelea kufanyika katika kumbi tofauti Manispaa ya Songea  na yanatarajia  kukamilika hapo kesho tarehe 26 oktoba mwaka huu.

Lengo la mafunzo hayo kwa wasimamizi wasaidizi wa vituo ni kutoa mwongozo na utaratibu wa kuzingatia wakati wa kuandaa kituo, kufungua kituo, kupiga kura,  kuhesabu kura, na kufunga kituo.

Msimamizi wa Uchaguzi Jimbo la Songea mjini  Tina Sekambo amesema “ ni muhimu wasimamizi na  wasaidizi wa vituo kuhakikisha kuwepo kwa utulivu na usalama katika kituo cha kupigia kura, akiyataja mafanikio ya uchaguzi yatatokana  utekelezaji wa  majukumu yako kwa kufanya kazi kwa weledi, uadilifu, kwa kuzingatia miongozo na maelekezo yanayotolewa na tume ili kuzuwia kusababisha vurugu, na malalamiko.”  Tina amesisitiza.

Tina alibainisha kuwa uchaguzi ni hatua na hutekelezwa kwa kufuata sheia hivyo aliwaasa wasimamizi wote wa vituo  wasifanye kazi kwa mazoea kwasababu kila hatua ya uchaguzi ni maelekezo ya sheria sio maamuzi  ya mtu binafsi.

Alisema Jimbo la Songea Mjini lina vituo 393 na kwa kila kituo kitakuwa na msimamizi wa kituo na wasaidizi wake ili kuweza  kusimamia uchaguzi vizuri kama maelekezo ya Tume yalivyoelekeza.

Aliwaaasa wasimamizi wa vituo na wasaidizi wake kuandaa kituo mapema iwezekanavyo na kuhakikisha kinafunguliwa saa 1:00 asubuhi   ikiwa pamoja  na kuweka kituturi sehemu salama ili mpiga kura aweze kupiga kura  kwa uhuru na haki.

Naye Afisa wa Tume ya Taifa ya uchaguzi Agatha Nchimbi amesema “ Tume imejipanga vizuri katika kuhakikisha zoezi hili linakwenda vizuri na vifaa vyote vya vinavyopaswa kuwepo kwenye kituo cha kupigia kura vinakuwepo, hata hivyo wasimamizi wote  wanapaswa  kuzingatia vipaumbele kwa wazee, walemavu, wagonjwa, wajawazito, na wanaonyonyesha.

Nao washiriki wa mafunzo hayo kwa nyakati tofauti walisema wamepokea mafunzo hayo na wameahidi kufuata maelekezo yote ya Tume ya Taifa ya Uchaguzi ili kufanikisha zoezi zima la uchaguzi mkuu unaotarajia kufanyika juma lijalo 28 oktoba mwaka huu.

MTAYARISHAJI;

AMINA PILLY;

AFISA HABARI MANISPAA YA SONGEA.

25 oktoba 20

 

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa