• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

WAZEE WALIA NA KERO YA MATIBABU

Tarehe ya kuwekwa: October 2nd, 2017

WAZEE WALIA NA KERO YA MATIBABU

WAZEE katika Halmashauri ya Manispaa ya Songea mkoani Ruvuma wameitaja kero ya kupata matibabu bure inaongoza kwa wazee hali ambayo inasababisha wazee wengi kukosa matibabu.

Akisoma risala ya wazee siku ya maadhimisho ya siku ya wazee duniani Oktoba mosi mwaka huu,Makamu Mwenyekiti wa Baraza Huru la Wazee wa Manispaa ya Songea Sophia Hasara,ameiomba serikali kuwapatia wazee kadi za matibabu bure kama ilivyoelezwa na serikali.

Amemuomba Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Songea kuharakisha mchakato wa upatikanaji wa kadi za matibabu bure kwa wazee wote wa Manispaa hiyo ili kumaliza kero hiyo ambayo inasababisha baadhi ya wazee kupoteza maisha kwa kushindwa kugharamia matibabu.Hata hivyo wazee hao wameipongeza serikali ya awamu ya tano chini ya Rais Dk.John Magufuli kuongeza bajeti ya Wizara ya Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto kwa mwaka wa fedha wa 2017/2018 ambapo wamesema bajeti hiyo pia itawanufaisha wazee wa Tanzania.

Katika risala yao wazee wamelaani matukio ya mauaji ya wazee,utekaji nyara wa watoto na mashambulio mbalimbali yanayotokea kwa viongozi na kwamba ili kukabiliana na matukio hayo wameshauri serikali kukaa na wazee ili waweze kupata mawazo ya nini cha kufanya  kuondoa taharuki hiyo.Wamesema ni wajibu wa serikali ya awamu ya tano kushirikisha wazee wa kada mbalimbali ili waweze kutumia ujuzi,uzoefu na michango ya mawazo kufanikisha malengo mbalimbali ya serikali.

Wamebainisha kuwa ingawa wazee hawana nguvu nyingi,hata hivyo kwa kutumia hekima na busara zao wanaweza kuelekeza,kushauri na kusimamia kwa ufanisi lengo kuu la awamu ya tano la kuwa na serikali ya viwanda ili kuleta maendeleo kwa watanzania.Wazee hao wamesisitiza mshikamano,umoja na juhudi ili kufikia lengo lililowekwa na serikali la hapa kazi tu na kusisitiza serikali itunge sheria ya wazee ili kuwezesha wazee kunufaika na sheria hiyo kwa kuwa sera ya wazee pekee yake haina uwezo wa kutatua changamoto za wazee.

“Sisi wazee wa Manispaa hatujanufaika lolote na sera ya Taifa ya wazee ya mwaka 2003 kwa sababu sera hiyo haina meno kwa kuwa haijatungiwa sheria’’,inasema risala ya wazee hao.Wamemuomba mgeni rasmi katika maadhimisho hayo Mbunge wa Songea mjini Leonidas Gama kuwafikishia kilio cha kutungwa sheria ya wazee Bungeni Dodoma na kwamba hawaoni sababu za msingi za kucheleweshewa kutungiwa sheria hiyo wakati sera imedumu muda mrefu.

Kulingana na takwimu za wazee za mwaka 2016,Manispaa ya Songea  ina zaidi ya wazee 11,000.Maadhimisho ya wazee ya mwaka 2017 ni ya 19 ambapo maadhimisho ya kwanza yalifanyika mwaka 1999,kauli mbiu ya mwaka huu ni Kuelekea Uchumi wa Viwanda,Tuthamini Mchango, Uzoefu na Ushiriki wa Wazee kwa Maendeleo ya Taifa.

Taarifa imetolewa na 

Albano Midelo,Afisa Habari Manispaa ya Songea

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa