• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

WAZIRI Kalemani akemea wanaohujumu miundombonu ya umeme Songea

Tarehe ya kuwekwa: April 5th, 2019

Waziri wa Nishati Dkt Medard Kalemani ametoa onyo kali kwa wanaohujumu miundombinu ya umeme nchini kote akisema serikali imedhamiria kupambana nao na kwamba hatua kali za kisheria zitachukuliwa dhidi ya watakaobainika.


Aliyasema hayo kwa nyakati tofauti jana, Aprili 3, 2019 akiwa katika ziara ya kazi mkoani Ruvuma, Wilaya ya Songea ambapo aliviwashia umeme vijiji vya Unangwa na Changarawe pamoja na kuzungumza na wananchi.


Aliwaomba wananchi kuwa wazalendo kwa kulinda miundombinu ya umeme iliyo katika maeneo yao na kuwafichua wale wanaoihujumu ili wachukuliwe hatua kwani wanarudisha nyuma jitihada za serikali kuwaletea wananchi maendeleo.


Akizungumzia tukio la kuhujumu miundombinu ya umeme lililotokea hivi karibuni eneo la Mlandizi na kusababisha ukosefu wa umeme kwa mikoa na wilaya kadhaa, hususani Dar es Salaam; Waziri alisema ameunda timu maalumu kuchunguza waliohusika ili hatua kali zichukuliwe dhidi yao.


Katika hatua nyingine, Waziri Kalemani alitoa maagizo kwa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) kutoa elimu ya kutosha kwa wananchi kuhusu utaratibu wanaopaswa kuufuata ili waunganishiwe umeme.


Alisema, katika ziara ambazo amekuwa akifanya maeneo mbalimbali nchini, amegundua wananchi wengi bado hawana uelewa wa utaratibu sahihi wanaopaswa kufanya ili wapate umeme hali inayosababisha wengi wao walalamike kutopewa huduma hiyo muhimu, wakidhani hawatendewi haki.


“Sehemu nyingi nimekutana na malalamiko ya wananchi wakidai hawajaunganishiwa umeme lakini ukifuatilia unabaini hawajalipia ndiyo maana hawajapatiwa huduma. TANESCO waelimisheni wananchi waelewe,” alisisitiza.


Akifafanua zaidi, alisema hata baadhi ya taasisi mbalimbali zikiwemo shule, vituo vya afya, masoko, miradi ya maji na nyinginezo, hususani zilizoko vijijini, kumekuwa na malalamiko ya kutounganishiwa umeme lakini baada ya kufuatilia imebainika wengi wao hawajalipia ndiyo maana hawajaunganishiwa.


Sambamba na kuhamasisha wananchi kulipia shilingi 27,000 ili waunganishiwe umeme, Waziri pia aliwahamasisha wale wenye nyumba zenye vyumba vichache watumie vifaa vya Umeme Tayari (UMETA) badala ya kutandaza nyaya (wiring) ili kupunguza gharama.


Alisema serikali imetoa vifaa hivyo 250 bure kwa kila eneo ambako wakandarasi wa umeme vijijini wanaendelea kuunganisha wananchi na kwamba idadi hiyo ikiisha vitauzwa kwa gharama ndogo ya shilingi 36,000 tu.


Katika ziara hiyo pia, Waziri alikagua miundombinu mbalimbali ya Mradi mkubwa wa umeme wa Makambako – Songea unaotarajiwa kuzinduliwa rasmi na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Magufuli, Jumamosi ya Aprili 6, mwaka huu mjini Songea.


Waziri alifuatana na viongozi pamoja na wataalamu mbalimbali kutoka wizarani, TANESCO na REA.


Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa