• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

WAZIRI Manyanya alivyoguswa na mwenye ulemavu wa viungo Nyasa,amkabidhi baiskeli

Tarehe ya kuwekwa: November 3rd, 2018

Mbunge wa jimbo la Nyasa Mhandisi stella Manyanya ambaye pia ni Naibu Waziri wa Viwanda Biashara na Uwekezaji amemkabidhi baiskeli yaenye thamani ya Tsh1,500,000/=( milioni moja laki tano) mlemavu wa miguu ikiwa ni ahadi yake aliyoitoa alipofanya ziara katika Kijiji cha malini kata ya Mtipwili Hivi karibuni Wilaya ya Nyasa Mkoani Ruvuma.

Baiskeli hiyo imekabidhiwa  na Katibu wa Mbunge Manyanya ndugu Cosmas Nyoni Nyumbani kwa John Mapunda ambaye ni mwenye ulemavu anayeishi katika kijiji cha Malini Kata ya Mtipwili Wilayani Wilaya ya Nyasa ili kumrahishisa mwenye ulemvu huyo wa viungo.

Manyanya alifafanua kuwa kwa kushirikiana na mwanae anayeitwa Hope exaveria ambaye pia ni mwenyeulemavu aliamumua kumsaidia baiskeli hiyo mwenye ulemavu  huyo kwa kuwa akiwa katika ziara yake alipokuwa kijiji cha Malimi alipokea ombi la Mwenye ulemavu huyo kuomba Baiskeli kwa kuwa alikuwa anapata shida ya kutembea na kubadilishana mawazo na wenzake hivyo baiskeli itamsaidia kutembea na kubadilishana mawazo na na ndugu wenzie.

Aliongeza kuwa anatambua  ulemavu kwa kuwa ana mtoto ambaye ni mwenye ulemavu na anaona walemavu nao ni binadamu kama walivyo binadamu wengine ambao wanahitaji upendo na kuthaminiwa ikiwa ni pamoja na kusaidiwa au kutatuliwa changamoto zao.

“Nimetumwa na Mbunge Stella Manyanya ili nikuletee baiskeli ambayo ulimuomba akiwa katika ziara katika kijiji hiki cha Malini kama tunavomfahamu Mbunge wetu kila anachoahidi anakitekeleza na leo hii amekuletea kwa kushirikiana na mwanae anayeitw Hope Exaveria ambaye naye ni mlemavu wamekubaliana kukusaidia wewe ili uweze kutembea vizuri na kubadilishana na mawazo na marafiki zako na ndugu jamaa na marafiki”alisema Katibu huyo wa Mbunge.

Akipokea msaada huo ndugu John Mapunda alimshukuru sana Mbunge na kusema kuwa kabla ya kupata baiskeli hiyo alikuwa anapata shida ya kutembea kwa kuwa alikuwa anatembea kwa kutambaa kwa shida lakini mara baada ya kupata baiskeli hiyo atapata fursa ya kuwatembelea ndugu jamaa na marafiki na wakati mwingine atakuwa akibadilishana mawazo na rafiki zake kijiweni.

Mh Manyanya amekuwa na kawaida ya kuwasaidia watu wenye mahitaji maalum na hivi karibuni akiwa katika ziara ya siku nane katika Tarafa ya Mpepo Katika Kijiji cha Lunyele Katika shule ya msingi Lunyele aliwasaidia ushauri wa matibabu kwa watoto watatu waliozaliwa katika familia tatu tofauti  na kumwagiza Mganga mkuu  wa Wilaya ya Nyasa Dkt Aroin Hyera kwenda kuwapa ushauri wa kitaalam watoto watatu ambao walizaliwa wakiwa na vichwa vikubwa wazazi wao wakiwa hawajui cha kufanya.

Naye mwenyekiti wa kijiji cha malini Kata ya Mtipwili alimshukuru sana kwa kuwajali na kuwasaidi wananchi wake wenye mahitaji maalum na kumwomba aendelee na moyo huo huo anao hawatamwangusha kwa kuyasema kwa wananchi miradi yote anayotekeleza kwa Wananchi.

IMETOLEWA NA

NETHO C.SICHALI

AFISA HABARI

WILAYA YA NYASA

0783662568

TAR.02/11/2018

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • Bil. 22.9 Kujenga Masoko ya Kisasa Manzese A na B, na Kiwanda cha Kuchakata Mazao ya Nafaka Lilambo

    July 06, 2025
  • MBUNGE SONGEA MJINI AKABIDHI KOMPYUTA NA KUFADHILI UKARABATI WA OFISI ZA POLISI

    June 27, 2025
  • DC Songea bAzindua Dawati la Huduma za Ustawi wa Jamii Stendi ya Mabasi Songea

    June 24, 2025
  • Meya Mbano; Amewataka Wananchi Kulinda Haki za Watoto

    June 16, 2025
  • Tazama zote

Video

Makabidhiano ya Mkataba Soko la Manzese A&B
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa