• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

WAZIRI MKUU AWATOA HOFU WAKAZI WA MANISPAA

Tarehe ya kuwekwa: January 9th, 2018

WAZIRI Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Kassim Majaliwa, amewatoa hofu Wakazi 1,000 wa eneo la Mwengemshndo Manispaa ya Songea wanaodai fidia ya Tshs. Bilioni 3.8  ya eneo lao ambalo limechukuliwa kwa ajili ya Ujenzi wa Viwanda.

Waziri Mkuu Amesema Serikali ya Awamu ya Tano inatambua kilio chao ambacho amesema ni cha muda mrefu na kwamba alishawahi kupata ombi maalum kutoka kwa Mbunge wao wa zamani, Bw. Leonidas Gama ambaye sasa ni marehemu.

...........“Alipotoka kutibiwa India alikuja ofisini kwangu na kunieleza kwamba ana mambo mawili ambayo nikifanya ziara mkoani Ruvuma anaomba niyatafutie ufumbuzi. La kwanza lilikuwa ni hili la fidia kwa wakazi wa Mwengemshindo, na la pili lilikuwa ni la Ujenzi wa Kituo cha Mabasi cha Mjini Songea”..alisema Majaliwa.

Waziri Mkuu Majaliwa aliwaeleza wakazi hao kwamba eneo hilo limetengwa na Manispaa kwa ajili ya ujenzi wa viwanda ambapo wawekezaji watatu tayari wamekwishajitokeza na wanataka kujenga Viwanda Vitatu.

“Kutakuwa na kiwanda cha kusindika Mahindi, kutengeneza Pumba za Kuku na Ng’ombe na Mbolea. Kiwanda cha pili kitakuwa ni cha kusindika Kahawa na cha tatu kitakuwa ni cha kukamua Mafuta ya Mbegumbegu,” alisema Waziri Mkuu.

Akitoa ufafanuzi kuhusu kuchelewa kwa malipo yao, Waziri Mkuu alisema kwamba katia ya wawekezaji hao watatu aliyekwishalipa fidia ni Mwekezaji mmoja tu, na kwamba kwa mujibu wa sheria ya uwekezaji, fidia inapaswa kulipwa na mnunuzi wa eneo husika.

 Hata hivyo, Waziri Mkuu alikiri kuwepo kwa mapungufu wakati wa ulipaji kwa sababu walifuata orodha ya majina (kialfabeti) badala ya kutoa malipo kwa wakazi wa eneo husika.

Ameongeza kuwa Mwekezaji anataka kuanza Ujenzi, lakini ndani ya eneo lake kuna watu ambao bado hawajalipwa, kwa hiyo hawawezi kutoka hadi wale waliobakia nao walipwe.

Ameahidi Serikali kuwafuatilia wawekezaji wengine ili nao walipe fedha zao haraka ili waliobakia waweze kulipwa

Jumla ya watu 2,179 walifanyiwa uthamini Mwaka 2008 na gharama yao kubainika kuwa ni zaidi ya shilingi bilioni   3.25 Kuanzia Juni 2015,ambapo Serikali iliwalipa wakazi 1,179 Kiasi cha zaidi ya shilingi bilioni 1.9  kati ya hizo,bilioni 1.2 zilikuwa ni Malipo ya thamani ya Mali za wananchi na zaidi ya milioni 710 zilikuwa ni RIBA kutokana na malipo hayo kuchelewa kufanyika.

Eneo la Mwengemshindo lenye ukubwa wa Hekta 2,033  lilitwaliwa na Mamlaka ya Ukanda Maalum wa Uwekezaji (EPZA) kwa kushirikiana na uongozi wa Mkoa wa Ruvuma, na Manispaa ya Songea tangu Mwaka 2007. Eneo hilo linajumuisha Mitaa ya Luwawasi (Mkuzo), Mwengemshindo na Luhira.

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • MWENGE WA UHURU WAPOKELEWA MKOANI RUVUMA

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma Awapongeza Wastaafu 86 wa Kada ya Ualimu Mkoani Ruvuma

    May 08, 2025
  • Kamati ya Siasa Wilaya Yaridhishwa na Hatua za Miradi ya Maendeleo

    May 06, 2025
  • Tazama zote

Video

YALIYOJIRI MAKABIDHIANO YA MBIO ZA MWENGE WA UHURU
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa