• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

WAZIRI NAPE ATOA WITO KWA WANANCHI MKOANI RUVUMA "KUTUMIA MAJINA YA WAASIS WETU KATIKA ANWANI ZA MAKAZI ILI KUWAENZI "

Tarehe ya kuwekwa: April 14th, 2022

Na,

AMINA PILLY,

AFISA HABARI MANISPAA.

14.04.2022

Waziri wa habari, mawasiliano na Teknolojia ya habari, Nape Moses Nnauye amewataka wananchi  kushirikiana na viongozi Mkoani Ruvuma kutumia zoezi la anwani za makazi kuwaenzi waasisi katika maeneo yao ili kulinda historia yao.

Nape aliyasema hayo hapo jana Aprili 13, 2022 katika ziara yake ya kukagua zoezi la anwani za makazi Mkoani Ruvuma ambapo ameelekeza kutumia zoezi hilo kwa kuenzi historia ya nchi kwa kutaja majina ya viongozi na maarufu katika maeneo ya mitaa na barabara kubwa kutokana na utendaji kazi wao katika kutengeneza historia ya nchi.

Alisema “Nimekuja Ruvuma kukagua na kuona zoezi hili linaendeleaje na nina furaha kubwa katika Mikoa inayofanya vizuri, Mkoa wa Ruvuma ni miongoni mwa mikoa inyofanya vizuri katika zoezi hili” Nape alibainisha.

Aidha, ametoa wito kwa Wakala wa barabara mijini (TANROADS) na Wakala wa barabara vijijini (TARURA) kushiriki kikamilifu katika zoezi hilo   kukamilika kwa wakati ili kusaidia kuweka majina na alama katika barabara zao.”Alisisitiza”

 Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma, Brigedia Generali Balozi Wilbert Ibuge amesema zoezi hilo  linaendelea vizuri na linatarajiwa kukamilika ifikapo Aprili 30, 2022 na hivyo umakini utaongezeka katika kukamilisha zoezi hilo kwa wakati.

Akitoa takwimu za Mkoa wa Ruvuma katika utekelezaji wa operesheni ya anwani za makazi kitaifa Afisa Tehama Mkoa wa Ruvuma Yahaya Madenge alisema kuwa, hadi sasa Mkoa wa Ruvuma umeshika nafasi ya kumi Kitaifa katika utekelezaji wa zoezi hilo kwa kufikia zaidi ya asilimia 96%.

Kwa upande wake Afisa Tehama Manispaa ya Songea, Mvano Mbalale alisema kuwa zoezi hilo kwa Halmashauri ya Mnaispaa ya Songea limefanyika kwa weledi mkubwa ambapo wananchi walitoa ushirikiano kwa wataalamu waliofanya zoezi la ukusanyaji wa  taarifa katika maeneo yao.

Akizungumza kwa niaba ya Mstahiki Meya wa Manispaa ya Songea, Mh. Diwani Jeremiah Milembe (Naibu Meya Manispaa ya Songea) alieleza kuwa zoezi hilo ndani ya Manispaa ya Songea litakamilika kabla ya  kufikia tarehe husika iliyopangwa na Mkoa na hivyo ametoa rai kwa wananchi wote kuendelea kutoa ushirikiano katika utekelezaji wa zoezi hilo.

Mwisho. 

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa