• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA AMEONGOZA BONANZA KUHAMASISHA SENSA.

Tarehe ya kuwekwa: August 21st, 2022

Na

Amina pilly

20 Agosti 2022

Waziri wa katiba na sheria Dkt. Damasi Ndumbaro amewataka wananchi wote wa Songea mjini kujitokeza katika zoezi la sensa itakayofanyika tarehe 23 agosti 2022.

Hayo yametamkwa jana tarehe 20 agosti 2022 katika uwanja wa majimaji iliyoshirikisha wananchi mbalimbali, wadau wa michezo, viongozi wa vyama vya siasa kwa lengo la kuhamasisha wananchi kujitokeza katika zoezi la sensa.

Dkt. Ndumbaro amesema kuwa sensa inaiwezesha serikali kupata takwimu sahihi zitakazo saidia katika upangaji wa mipango ya maendeleo ya mji wa songea na taifa kwa ujumla, ambapo alisema  kuwa “sensa ni ajenda yetu kwa mwaka huu ambayo itawezesha kupata takwimu ya ongezeko la watu ambapo itasaidia kupandisha hadhi ya mji kutoka Manispaa na kwenda kuwa jiji”.



 Alisema makarani wote watakaohusika katika zoezi la sensa wahakikishe wanatekeleza wajibu wao kwa kuzingatia mafunzo waliyopewa  ili  kufanikisha ukusanyaji wa  takwimu sahihi unafanikiwa kwa kiasi kikubwa.

Aliongeza kuwa michezo ni muhimu na inasaidia kujenga afya ya mwili hivyo amewataka wananchi kuendelea kufanya mazoezi kwa  kila mwisho wa mwezi ambapo amewaondoa shaka wanamichezo wa  timu mbalimbali zinazoshiriki mazoezi ambapo ameahidi  kuwa mlezi wa timu hizo kwa kusaidia vitu muhimu kama jezi, mpira na t-shirt kwa lengo la kuwaunga mkono SOMI FOUNDATION 2022 SENSA MARATHON ambayo ni imeanzishwa na jamii ya Songea kwa madhumuni ya kudumisha michezo  na mazoezi ya viungo vya mwili na shughuli nyinginezo za kijamii.

Aidha Dkt. Ndumbaro ( MB) ametoa T-shirt  kwa SOMI FOUNDATION na washiriki wote waliohudhuria kwenye mazoezi, Mipira Miwili kwa timu  za Mpira wa Miguu na kikapu pamoja na Medali kwa wanamazoezi hao. 

Naye mbunge wa viti maalumu Ruvuma Mhe. Mariamu Nyoka, amewarai wananchi kujitoa katika zoezi la sensa na kutoa taarifa sahihi ili kufanikisha Serikali kupata takwimu sahihi ambazo zitasaidia  katika utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo mkoani Ruvuma na taifa kwa ujumla.

Mheshimiwa  Mariamu (MB) alisema katika kuunga mkono jitihada za Mheshimiwa Mbunge Dkt. Ndumbaro  ametoa zawadi mbalimbali zinazohusisha vifaa vya michezo kwa dhumuni la kuhamasisha wananchi kushiriki katika michezo, na kuwahamasisha kujitokeza katika zoezi la sense ambapo miongoni mwa zawadi zilizotolewa ni pamoja na bibs seti mbili, jezi seti mbili, mpira wa basketball mmoja na mipira ya netball miwili za timu mbili za wanawake, pamoja na  mipira ya miguu miwili  na jezi za timu mbili za wanaume.

Wananchi nao kwa wakati tofauti, wamewapongeza waheshimiwa wabunge hao  kwa kuhamasisha  jamii kufanya mazoezi ambayo imehusisha uhamasishaji wa Sensa kwa wananchi kujitokeze kuhesabiwa tarehe 23 agosti 2022 ambapo kwa umoja wao wameahidi kujitokeza kuhesabiwa.  

MWISHO


Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa