• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

WILAYA ya Nyasa yatoa zaidi ya milioni 35 kwa wajasirimali wadogo

Tarehe ya kuwekwa: July 3rd, 2019

Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa imetoa shilingi milioni thelathini na tano laki saba themanini na sita elfu mia nne tisini na mbili (35,786,492/=) kukopesha vikundi kumi na mbili (12) vya wanawake, vijana na walemavu ikiwa ni asilimia kumi (10%) ya mapato ya ndani ya Halmashauri.

Akiongea na wanufaika wa mikopo hiyo ofisini kwake, Mkurugenzi Mtendaji Wilaya ya Nyasa, Ndugu Jimson Mhagama amewataka wana vikundi hao kuzitumia fedha hizo vizuri kwa kuboresha shughuli mbali mbali za kiuchumi ili waweze kuzirudisha kwa wakati na ziendelee kukopeshwa kwa vikundi vingine vya ujasiriamali na kuinua uchumi wa wananchi wa Wilaya ya Nyasa.

Mhagama alifafanua kuwa Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa, kwa mwaka wa Fedha wa 2018/2019, imetenga bajeti ya shilingi 42,081,692/= kwa ajili ya kukopesha vikundi vya kina mama, vijana na walemavu ikiwa ni asilimia kumi ya mapato ya ndani kama ilivyoagizwa na Waziri wa Nchi Ofisi ya Tawala za Serikali za Mitaa kupitia Tangazo la Serikali Namba 286 la tarehe 5/4/2019 ambayo imeainisha utoaji na usimamizi wa mikopo kwa vikundi vya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu katika Serikali za Mitaa ambapo inazitaka Halmashauri zote kutenga asilimia kumi (10%) ya mapato yake ya ndani kuwezesha vikundi hivyo.

“Wilaya ya Nyasa tumefanikiwa kuto fedha zote tulizoweka kwenye Bajeti ya mwaka huu wa Fedha na tayari tumesha waingizia kwenye akaunti zenu za vikundi. Nawakumbusha Fedha hizi sio Ruzuku, huu ni mkopo na zinatakiwa kurudishwa ili na vikundi vingine viweze kunufaika na fedha mtakazorudisha”, alisema Mkurugenzi huyo.

Alivitaja Vikundi vya wanawake vilivyopewa mikopo hiyo kuwa ni, Amani (Kata ya Chiwanda), Chakula barafu (Kata ya Mbamba-bay), Umoja Group (Kata ya Mpepo), Acha Tuanze (Kata ya Lumeme), Umoja (Kata ya Kihagara) na Upendo Kiwono (Kata ya Mpepo).

Vikundi vingine ni vya vijana wa Kisasa (Kata ya Luhangarasi), Pikipiki (Kata ya Tingi), Tuungane Pamoja (Kata ya Liwundi), Dhahabu Kijani (Kata ya Mipotopoto) na Kikuso (Kata ya Mpepo) na kikundi kimoja cha walemavu cha Tuthaminiwe kutoka Kata ya Lipingo wilayani hapa.

Aidha alisema kila kikundi kimekopeshwa Tsh milioni tatu (3,000,000/=), kwa vikundi vya kina mama na vijana na kikundi cha walemavu kimekopeshwa shilingi 2,786,492/= (milioni mbili laki saba themanini na sita elfu mia nne tisini na mbili), ambayo watarudisha bila riba kwa kipindi cha mwaka mmoja.

Aliongeza kuwa tayari Halmashauri kwa kipindi cha robo ya kwanza imetoa shilingi 6,295,200/= kwa ajili ya vikundi vitatu vya Mamanilee, Upendo na Muongozo cha vijana wa Kata ya Lipingo.

Baadhi ya wanufaika wa mikopo hiyo, Mwenyekiti wa kikundi cha pikipiki kutoka Kata ya Tingi, walisema wanaipongeza sana Serikali kwa kuwajali makundi maalum hasa ya vijana kina mama na watu wenye Ulemavu kwa kuwa makundi hayo ndio hasa yanayo shughulika na utafutaji mitaji kwa kuwa Serikali imewapa mitaji hawata iangusha kwa kuwa watalipa kwa wakati kukuza uchumi katika jamii.

“Nachukua fursa hii kukupongeza sana Mkurugenzi wetu kwa kutupatia mikopo hii kwa kuwa makundi haya ndiyo haswa tunaohangaika kutafuta mitaji na hakuna mwaka ambao Halmashauri hii imetoa mikopo kwa vikundi kumi na tano, hayo ni maajabu. Sisi wanufaika hatuta kuangusha, tutafanya biashara vizuri na tutarudisha kwa wakati ili vukundi vingine vipewe mikopo hii isiyo na Riba”.

Aliongeza kuwa tayari Halmashauri kwa kipindi cha robo ya kwanza ilishatoa shilingi 6,295,200/= kwa ajili ya Vikundi vitatu vya Mamanilee, Upendo na Muongozo cha vijana wa Kata ya Lipingo.

IMEANDALIWA NA

NETHO CREDO SICHALI

AFISA HABARI

NYASA DC.O767417597

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa