• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

YALIYOJILI KAMPENI YA USAFI WA MAZINGIRA "USICHUKULIE POA NYUMBA NI CHOO"

Tarehe ya kuwekwa: June 29th, 2021

Halmashauri ya Manispaa ya Songea  ni  kati ya Halmashauri 8 za mkoa wa Ruvuma yenye  jumla ya wakazi 281,217  ikiwa wanaume 132,171 na wanawake  149,046.

Ikiwasilisha  taarifa ya hali ya kampeni ya kitaifa ya usafi wa mazingira katika Halmashauri ya Manispaa ya Songea hadi  mwezi Machi 2021 kwenye kikao cha wajumbe wa kamati ya maji na usafi wa mazingira, watendaji wa kata na maafisa afya wa kata pamoja na wadau mbalimbali wa usafi na mazingira,  katika ukumbi wa Manispaa ya Songea tarehe 24 Juni 2021.

 Afisa afya wa Manispaa ya Songea Maxensius Mahundi alisema  kampeni ya kitaifa ya usafi wa mazingira ndani ya Manispaa ya Songea kuanzia mwaka 2012/2013 hadi mwaka 2020/2021 ni pamoja na kufanya mikutano ya uhamasishaji (kuchefua) na ufuatiliaji katika jamii kwa mitaa yote 95, kutoa mafunzo elekezi kwa mafundi uwashi 51 kwa lengo la kuelimisha jamii juu ya ujenzi wa vyoo bora, kuendesha mashindano ya afya na usafi wa mazingira kwa kata 21 na kukusanya takwimu za hali halisi ya usafi wa mazingira katika kata zote zilizopo Halmashauri ya Manispaa ya Songea kwa kipindi cha kila robo mwaka.

Awali yalitolewa mafunzo kuhusu kampeni ya kitaifa ya usafi wa mazingira kwa waratibu elimu kata 21 juu ya ukarabati, ujenzi wa vyoo na uwekaji wa miundo mbinu ya kunawa mikono nje ya vyoo katika kipindi cha kila robo mwaka. “Alieleza”

Miongoni mwa changamoto zinazowakabili  katika utekelezaji  wa kampeni ya afya na usafi wa mazingira ni pamoja na wananchi kutojenga vyoo bora,  kutoweka miundo mbinu ya kunawa mikono nje ya choo kwa hiyari bali huhitaji shuruti,  kutokuwepo kwa uzio katika shule nyingi za msingi,   baadhi ya wakazi  huharibu miundombinu ya vyoo vya shule kwa  kuiba mabomba ya kutolea hewa chafu kutoka kwenye vyoo, ukosefu wa maji ya kudumu kwa baadhi  ya shule za msingi pamoja na ukosefu wa usafiri wa uhakika kwa watumishi wa ngazi ya kata kwa ajili ya kufanya ufuatiliaji wa shughuli za kampeni ya kitaifa ya usafi wa mazingira.”Mahundi Alibainisha”

Akizungumza kwa niaba ya Mkurugenzi wa Manispaa ya Songea Phillipo Beno alisema kwamba Halmashauri imejipanga kuimarisha usimamizi na ufuatiliaji wa usafi wa mazingira, kuhamasisha jamii kuweka ulinzi shirikishi na kuweka uzio katika shule, kufanya ukaguzi na kubainisha kaya zisizo na vyoo bora katika mitaa, pamoja na kuendelea kuwachukulia hatua za kisheria wakazi wa Manispaa ya Songea wasio na vyoo, wenye vyoo vibovu, wasioweka miundombinu ya kunawa mikono nje ya choo.‘Alisisitiza’

Hadi sasa jumla ya kaya 63,913 ambayo ni sawa na asilimia 100% katika Manispaa ya Songea  ambazo zimefikiwa na kampeni ya usafi wa mazingira tayari zina vyoo ambapo katika kaya hizo, kaya 57,458 sawa na asilimia 89.9% zenye vyoo bora  na kaya 6,455 sawa na asilimia 10.1%  ambazo bado hazina vyoo bora.

“USICHUKULIE POA NYUMBA NI CHOO”

IMEANDALIWA NA,

AMINA PILLY,

AFISA HABARI MANISPAA,

29.06.2021.

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa